Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimetoa wito kwa Jeshi la Polisi kufafanua tuhuma zinazomkabili aiyekuwa Meya wa Ubungo ,Boniface Jacob maarufu Boni Yai na kuhakikisha uchunguzi unafanywa ka uwazi , huku sheria ikifuata mkondo wake .
Pia kimetaka sheria na taratibu zizingatiwe katika mchakato wa ukamataji , ili zizinatiwe katika mchakato wa ukamataji ili kuunguza taharuki kwa wananchi .
Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC Anna Henga amesema hayo katika taarifa iliyotolewa Jumatano Septemba 18 ,2024 .
Msemaji wa Jeshi la Polisi David misime katika taarifa aliyoitoa leo Septemba 18 ,2024 amesema Jeshi la Polisi limemkamata na linamshikilia Jacob , mkazi wa Mbezi Msakuzi jijini Dar es Salaam kutokaana na makosa ya kujinai anayotuhumiwa nayo .
Boni yai amekamatwa leo Septemba 18 ,2024 akiwa maeneo ya Sinza jijini Dar es Salaam kwa mujibu wa wakili wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA ) Hekima Mwasipu anayemwakilisha Jacob ambaye ni kada ya Chama hicho .
Reviewed by KUSAGANEWS
on
September 19, 2024
Rating:


No comments:
Post a Comment