Kikosi cha Yanga kwa kundi la pili limepaa leo Alfajiri kuifwata CBE SA ya Ethiopia kwa ajili ya mchezo wa mkondo wa kwanza wa raundi ya pili ya ligi ya Mabingwa Afrika.
Wachezaji walioondoka leo ni wale ambao walikuwa hawana majukumu kwenye timu zao za taifa ,wakati mastaa kama Diarra ,Dube ,Aucho , Duke waliripotiwa kutua nchini Ethiopia jana .
Clatous Chama pamoja na Kenedy Musonda wanatarajiwa kufika nchini humo leo wakiwa wanaungana na wachezaji wa Yanga waliokuwa kwenye kikosi cha Taifa Stars , kilichocheza mchezo wa kufuzu Kombe la Mataifa Afrika dhidi ya Guinea juzi na kushinda mabao 2-1
BAADHI YA MASTAA YANGA WATUA ETHIOPIA ,KUKIPIGA NA CBE .
Reviewed by KUSAGANEWS
on
September 12, 2024
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
September 12, 2024
Rating:


No comments:
Post a Comment