WANANCHI WAVAMIA KITUO CHA POLISI KUSAKA WATUHUMIWA ,WAWILI WAFARIKI DUNIA .













Watu wawili  akiwemo mwanafunzi wa kidato cha nne wamepoteza maisha baada ya  kudaiwa kuvamia kituo cha Polisi lulembela wakitaka kuwadhuru watu waliodaiwa kuwa ni wezi wa watoto . 


Taarifa iliyowekwa na Msemaji wa Jeshi la polisi usiku huu ,David Misime ,inasema vurugu hizo zimetokea jana  Jumatano  Septemba 11,2024 saaa 8;30 mchana huko Lulembelea Wilayani Mbogwe mkoani Geita .


Amesema katika vurugu hizo ,waliooteza maisha ni mwanaume mmoja ambaye jina lake halijafahamika anaekadiriwa kuwa na miaka 18-20 na mwanafunzi wa kidato cha nne wa shule ya Sekondari Lulembela ,Theresia John (18)ambaye nyumba yao  inatazamana na kituo cha polisi .


Misime amesema chanzo cha vurugu hizo ni baada ya watu wawili kuonekana wakiwa wamebeba watoto wawili na wananchi waliokuwa kwenye mnada wa Lulembelea  kuwahisi kuwa ni wezi wa watoto na kuanza  kuwashambulia .

WANANCHI WAVAMIA KITUO CHA POLISI KUSAKA WATUHUMIWA ,WAWILI WAFARIKI DUNIA . WANANCHI WAVAMIA KITUO CHA POLISI KUSAKA WATUHUMIWA ,WAWILI WAFARIKI DUNIA . Reviewed by KUSAGANEWS on September 12, 2024 Rating: 5

No comments: