Bingwa wa kombe la Ligi kuu Tanzania Bara ,Yanga leo inaanza kampeni ya kutetea taji hilo ugenini dhidi ya Kagera Sugar.
Mchezo huu utafanyika kwenye uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.
Katika mchezo wa mwisho wa Ligi kuu timu hizo kukutana Mei 8 mwaka huu kwenye uwanja wa Azam Complex ,Dar es Salaam Yanga ilishinda kwa bao 1-0
Mchezo mwingine wa Ligi kuu leo KMC itakuwa wenyeji Coastal Union kwenye uwanja wa KMC Complex ,Kinondoni Dar es Salaam.
KMC na Coastal Union zilitok suluhu katika mchezo wa mwish wa Ligi katika timu hizo Mei 28 mwaka huu.
Kwenye uwanja wa Majaliwa ,Lindi wenyeji Namungo itaikaribisha Fountain Gate .
Yanga ,Coastal Union na Azam ambayo imecheza Agosti 28 ,2024 dhidi ya JKT Tanzania zimechelewa kuanza ligi kutokana na majukumu ya kimataifa .
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 29, 2024
Rating:


No comments:
Post a Comment