WASIOFAHAMIKA WAUA MMOJA WAJERUHIWA MKE ,WATOTO.











Watu wasiofahamika wamemuuwa mkazi wa Dodoma Micheal Richard (26) mkewe na watoto wawili wamejeruhiwa na nyumba waliyokuwa wakiishi imechomwa moto.


    Waliojeruhiwa na kulazwa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma ni mke  wa Micheal ,Agnes Eliah na watoto Ezra Micheal ,Witness Micheal ,Ephahim Micheal na mtoto mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu ambaye yeye aliathiriwa na moshi.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dododma ,George  Katabazi alisema tukio hilo limetokea Agosti 28, 2024 saa 9;00 alfajiri. Kamanda katabazi alisema uchunguzi wa awali unaonesha Micheal alivamiwa nyumbani kwake eneo la mtaa wa Mbuyuni ,kata ya Kizota na kuuawa kw kupigwa kichwani na kitu chenye ncha butu.

WASIOFAHAMIKA WAUA MMOJA WAJERUHIWA MKE ,WATOTO. WASIOFAHAMIKA  WAUA MMOJA WAJERUHIWA MKE ,WATOTO. Reviewed by KUSAGANEWS on August 29, 2024 Rating: 5

No comments: