Ester Nyahonge, mkazi
wa Mahina mkoani hapa amedai uzembe wa wauguzi Hospitali ya Wilaya Nyamagana
umesababisha kifo cha mwanaye aliyefariki dunia leo Jumapili Novemba 4, 2018
saa chache baada ya kuzaliwa
Akizungumza hospitalini hapo leo Ester amesema alikuwa akiwaita
wauguzi baada ya kupata uchungu lakini walimpuuza na kumtolea maneno ya kejeli
wakishangazwa na uamuzi wake wa kwenda katika hospitali hiyo
"Nilikuwa najisikia vibaya nawaita manesi ila wananipuuzia
wakisema nimekujaje hapa mpaka nikawa nasaidiwa na wajawazito wenzangu,”
amesema Ester.
“Nilijifungua mwenyewe
kisha ndio wakakurupuka wakijidai kunisaidia kumbe mtoto alikuwa ameshafariki.”
Tungaraza Njugu, mume wake Ester amedai alimpeleka mkewe
hospitalini hapo saa nane usiku lakini uzembe wa wauguzi ndio umesababisha kifo
cha mtoto wao wa kiume
Mganga Mkuu Mwanza, Dk Juma Mfanga amethibitisha kutokea kwa
tukio hilo na kwamba taratibu zinaendelea ikiwa ni pamoja na kuwahoji wauguzi
waliokuwa zamu katika wodi ya wajawazito
Mama ajifungua mtoto afariki, alaumu wauguzi
Reviewed by KUSAGANEWS
on
November 04, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
November 04, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment