Maaskofu waomba kukutana na Magufuli

Dar es Salaam. Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) wameomba kukutana na Rais John Magufuli ili kumueleza changamoto zinazowakabili

Kauli hiyo imetolewa leo Novemba 4, 2018 na Rais wa baraza hilo, Gervas Nyaisonga katika maadhimisho ya miaka 150 tangu ukatoliki uingie Tanzania Bara kupitia mji mkongwe wa Bagamoyo na miaka 100 tangu Kanisa Katoliki lipate padri wa kwanza mzawa yaliyofanyika Bagamoyo mkoani Pwani

Nyaisonga amesema zipo changamoto zinazowakabili lakini wataziwasilisha kwa Rais Magufuli watakapopata nafasi ya kukutana naye

"Hata nasi zipo changamoto zinazotukabili tunaomba nafasi ya kukuona na kukushirikisha yale tunayoona ili kupata mwanga wa utatuzi kwa hekima zako," amesema Askofu Nyaisonga

Amebainisha kuwa katika kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wake, Rais Magufuli ameonyesha kuwa ni mtu anayependa maendeleo na kusimamia haki

Amesema kwa kuwa hakuna masika yasiyo na mbu, zipo changamoto zinazomkabili katika uongozi wake hivyo wanamuombea

"Sisi maaskofu tunakupa pole na kukuombea sala kwa changamoto hizo," alisema
 
 
 

 
Maaskofu waomba kukutana na Magufuli Maaskofu waomba kukutana na Magufuli Reviewed by KUSAGANEWS on November 04, 2018 Rating: 5

No comments: