Zitto Kabwe akamatwa na Polisi Leo Dar Es Salaam ,Muliro Athibitisha


Jeshi la Polisi Mkoa wa kipolisi Kinondoni leo Jumatano Oktoba 31, 2018 limemkamata kiongozi wa chama cha ACT- Wazalendo, Zitto Kabwe

Kamanda wa polisi wa mkoa huo wa kipolisi,  Jumanne Murilo amethibitisha kukamatwa kwa mwanasiasa huyo ambaye pia ni mbunge wa Kigoma Mjini na kwamba anahojiwa katika kituo cha polisi Oysterbay

“Ni kweli tumemkamata  tunaendelea na mahojiano naye,” amesema Murilo na alipoulizwa sababu za kumkamata amesema, “Taarifa za kina tutatoa baadaye.”

Jana, Jeshi la Polisi mkoani Kigoma lilimtaka Zitto kuwasilisha vielelezo juu ya kauli aliyoitoa mbele ya waandishi wa habari Jumapili iliyopita Oktoba 28, 2018 kuwa ana taarifa za wananchi zaidi ya 100 kuuawa katika tukio la mapigano ya wananchi wa jamii ya Wanyantuzu na polisi wilaya ya Uvinza mkoani humo

Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma, Martin Ottieno amesema tuhuma za mbunge huyo hazina ukweli wowote na kusisitiza kuwa ni upotoshaji unaofanywa na wanasiasa

Zitto Kabwe akamatwa na Polisi Leo Dar Es Salaam ,Muliro Athibitisha Zitto Kabwe akamatwa na Polisi Leo Dar Es Salaam ,Muliro Athibitisha Reviewed by KUSAGANEWS on October 31, 2018 Rating: 5

No comments: