Baada ya kuhojiwa kwa saa tatu katika kutuo cha polisi
Oysterbay jijini hapa, mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe
amehamishiwa Kituo Kikuu cha Polisi kwa mahojiano zaidi
Leo Jumatano Oktoba 31, 2018 Jeshi la Polisi Mkoa wa
kipolisi Kinondoni lilithibitisha kumkamata mbunge huyo wa Kigoma Mjini
Akizungumza wakili wa mwanasiasa huyo Jebra Kambole
amesema baada ya mahojiano hayo, mteja wake ameelezwa kuwa anapelekwa Kituo
Kikuu cha Polisi kwa mahojiano zaidi
Mwananchi limeshuhudia mbunge huyo akifikishwa kituoni hapo
leo saa 10:10 jioni
Awali, Kamanda wa polisi wa mkoa huo wa kipolisi,
Jumanne Murilo alilieleza Mwananchi kuwa mbunge huyo amekamatwa na
kubainisha kuwa alikuwa akihojiwa kituo cha polisi Oysterbay
“Ni kweli tumemkamata tunaendelea na mahojiano naye,”
amesema Murilo na alipoulizwa sababu za kumkamata amesema, “Taarifa za kina
tutatoa baadaye.”
Jana, Jeshi la Polisi mkoani Kigoma lilimtaka Zitto
kuwasilisha vielelezo juu ya kauli aliyoitoa mbele ya waandishi wa habari
Jumapili iliyopita Oktoba 28, 2018 kuwa ana taarifa za wananchi zaidi ya 100
kuuawa katika tukio la mapigano ya wananchi wa jamii ya Wanyantuzu na polisi
wilaya ya Uvinza mkoani humo
Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma, Martin Ottieno amesema
tuhuma za mbunge huyo hazina ukweli wowote na kusisitiza kuwa ni upotoshaji
unaofanywa na wanasiasa
Zitto ahamishiwa Kituo Kikuu cha Polisi
Reviewed by KUSAGANEWS
on
October 31, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
October 31, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment