Happy Lazaro,arusha.
Zaidi ya wakulima mia mbili
wanatarajiwa kunufaika na elimu ya kilimo biashara na kuondokana na
kilimo cha mazoea na kuweza kuongeza pato la uchumi zaidi.
Aidha elimu hiyo tayari
imeanza kutolewa na Chama cha Wakulima wa Maua,Matunda na
Mbogamboga(TAHA) kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa kilimo Kwa baadhi ya
wakulima ambao Ndio wanatarajiwa kuwa mabalozi katika maeneo yao Kwa
kuwaunganisha wakulima pamoja na kutoa mafunzo hayo.
Aidha mafunzo hayo ambayo yametolewa
Kwa awamu mbili yalianza tangu febuari mwaka huu hadi sasa hivi ambapo wakulima
12 wamefuzu kuwa wakufunzi wa wakulima wengine baada ya kufikia vigezo
vinavyotakiwa.
Hayo yalisemwa Jana na Meneja mkuu
wa maendeleo kutoka Taha, Anthony Chamanga wakati akizungumza katika hafla ya
kuwakabithi vyeti wakufunzi hao ambao wataenda kuwa walimu wa wakulima wenzao
waliopo vijijini katika maeneo wanayotokea.
Chamanga alisema kuwa, wakulima
wengi wana uelewa wa kutosha juu ya kulima kisasa, kuzalisha na kutumia
teknolojia lakini changamoto kubwa ipo kwenye elimu ya biashara na masoko hali
iliyowalazimu kutafuta wadau mbalimbali katika kusaidiana kutafuta ufumbuzi wa
changamoto hiyo.
"lengo kubwa la mafunzo hayo ya
kilimo biashara ni kuhakikisha kila mkulima anaondokana na kilimo cha mazoea na
kupitia wakufunzi hawa tunatarajia kila mmoja afikie wakulima mia mbili kwa
mwaka ambapo wakulima hawa wametoka maeneo mbalimbali ikiwemo Arusha, Manyara,
Zanzibar, na Kilimanjaro . "alisema Chamanga.
Kwa upande wa mmoja wa wafadhili wa
mafunzo hayo, ambaye ni Mshauri Janneke Beemster kutoka shirika la Trias
linalojihusisha na kuwajengea uwezo wakulima na wafugaji alisema kuwa,
wameshirikiana na Taha kuhakikisha wanapata wakulima hao ambao waliwapatia
mafunzo hayo na Hivi sasa wamekuwa wakufunzi.
Alisema kuwa, matarajio yao ni
kuhakikisha mafunzo hayo yanaleta matokeo mazuri kwa wakulima ili waweze kulima
kilimo cha biashara na kuondokana na kilimo cha mazoea walichonacho na kupitia
wakufunzi hao wataleta mabadiliko makubwa kwani wao ndio wanategemewa kuwafikia
wakulima wenzao kutokana na mbinu walizofundishwa.
Kwa upande wa Mshauri mwingine
kutoka shirika linalosaidia wakulima na wafugaji la Aha, Barbara Pichler
alisema kuwa, wamekuwa wakishirikiana Kwa pamoja kuwezesha wakulima na kuongeza
ujuzi katika ujasiriamali, na kuwa na uwezo zaidi katika eneo lao la
biashara.
Baadhi ya wakulima waliohitimu
mafunzo hayo kutoka mkoani Kilimanjaro , Hashimu Abdalah na Clemence
Makundi kutoka Arumeru walisema kuwa, wameweza kujifunza mbinu mbalimbali za
kilimobiashara na kupata uelewa mkubwa wa mambo ambayo walikuwa hawayafahamu
hapo awali, hivyo wataenda kuwa mabalozi wa wakulima wengine katika maeneo yao.
Zaidi ya wakulima mia mbili kunufaika na elimu ya kilimo biashara.
Reviewed by KUSAGANEWS
on
October 31, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
October 31, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment