IGP SIRRO AWATAKA WANANCHI WA UVINZA MKOANI KIGOMA KUENDELEA KUTOA TAARIFA SAHIHI ZITAKAZOFANIKISHA KUWAKAMATA WALIOJIHUSISHA NA MAUAJI YA ASKARI POLISI

Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akizungumza na baadhi ya wananchi wa Wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma, wakati alipofanya ziara mkoani humo Jana 24/10/2018 na kuwataka wananchi kuendelea kutoa taarifa sahihi zitakazofanikisha kukamatwa kwa watu waliojihusisha na tukio la kuwashambulia na kuwaua askari wawili na wananchi wawili wilayani humo. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akisalimiana na Mkuu wa wilaya ya Uvinza Mhe. Mwanamvua Mlindoko, wakati alipowasilia wilayani Uvinza Tarafa ya Nguruka mkoani Kigoma Jana 24/10/2018, kwa lengo la kuzungumza na wananchi kufuatia tukio la kushambuliwa na kuuawa kwa askari wawili na wingine mmoja kujeruhiwa wakati wakitekeleza zoezi la kuwaondoa wananchi waliovamia eneo la Ufugaji Ranchi ya Taifa NARCO kwa kuendesha shughuli za kilimo kinyume cha sheria na taratibu za nchi. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akizungumza na wananchi (hawapo Pichani) wa Tarafa ya Nguruka wilayani Uvinza mkoani Kigoma Jana 24/10/2018, na kuwataka kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kufichua uhalifu na wahalifu pamoja na watu wanaojihusisha na matukio ya mauaji ili waweze kuchukuliwa hatua kali za kisheria. Picha na Jeshi la Polisi.

Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akiondoka baada ya kumaliza mkutano na wananchi wa Tarafa ya Nguruka wilayani Uvinza mkoani Kigoma Jana 24/10/2018, ambapo IGP Sirro, aliwataka wananchi kuendelea kutoa taarifa sahihi zitakazofanikisha kukamatwa kwa watu waliojihusisha na tukio la kuwashambulia na kuwaua askari wawili na wananchi wawili wilayani humo. Picha na Jeshi la Polisi.


IGP SIRRO AWATAKA WANANCHI WA UVINZA MKOANI KIGOMA KUENDELEA KUTOA TAARIFA SAHIHI ZITAKAZOFANIKISHA KUWAKAMATA WALIOJIHUSISHA NA MAUAJI YA ASKARI POLISI IGP SIRRO AWATAKA WANANCHI WA UVINZA MKOANI KIGOMA KUENDELEA KUTOA TAARIFA SAHIHI ZITAKAZOFANIKISHA KUWAKAMATA WALIOJIHUSISHA NA MAUAJI YA ASKARI POLISI Reviewed by KUSAGANEWS on October 25, 2018 Rating: 5

No comments: