Watumishi tisa wa soko la kwa Sadala akiwemo mkuu wa
soko ilo Bw. Joseph Akyoo wamekamatwa na maafisa wa TAKUKURU
kwa kushirikinana na jeshi la polisi katika mkutano wa hadhara
wakituhumiwa kuharibu mashine za kutolea risiti za EFDs na kutumia
risiti bandia kukusanya ushuru katika soko hilo hali iliyotajwa
kuisababishia hasara serikali
Watumishi hao wa soko hilo wamekamatwa baada ya
kuibuka kwa tuhuma kutoka kwa maelfu ya wafanyabiashara mbele ya mkutano
na kudai kuwa wamekuwa wakipewa risiti feki za kuandika kwa mkono na kuchukua
fedha ambazo hazifiki halmashauri lakini pamoja na kutoa fedha hizo bado
mazingira ya soko ilo bado ya uchafu uliyokithiri
Baada ya kusikia tuhuma hizo kutoka kwa wafanyabiasha
mkuu wa wilaya ya Hai Bw.Lengai Ole Sabaya akatoa maelekezo ya serikali
na kutaka watuhumiwa washikiliwe ili kupisha uchunguzi
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Hai
Yohana Sinto amesema matukio ya ubadhilifu wa risiti unachangia
kuikoseshaserikali mapato huku akiahidi kutatua tatizo sugu la uchafu
ulilokithiri kwenye soko hilo.
Watumishi 9 mbaroni kwa Kufoji Risiti za EFDs
Reviewed by KUSAGANEWS
on
October 06, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
October 06, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment