Mkuu wa mkoa wa
Arusha Mrisho Gambo amesema kuwa mkoa huo hata kama utakuwa wa mwisho katika
ufaulu kitaifa lakini suala la wizi wa mitihani lipigwe vita kwa nguvu zote
sanjari na udanyanyifu katika masomo kwani inawajenga wanafunzi kuwa sio
waadilifu siku za usoni.
Gambo ameyasema hayo
wakati wa mahafali ya Kidato cha nne kwa shule zote za serikali na binafsi za
jiji la Arusha zilizofanyika kiwilaya katika uwanja wa sheikh Amri Abeid
jijini hapa na kuwataka viongozi wote katika mkoa huo kupiga vita udanganyifu
wowote katika masuala
Aidha kwa upande
wake Afisa Elimu jiji la Arusha Valentine Makuka amesema kuwa halmashauri ya
jiji hilo iliona kuna baadhi ya wanafunzi hawana uwezo wa kumudu gharama za
kusherehekea mahafali hivyo kuja na utaratibu huo ambao utasaidia watoto wasio
na uwezo nao kujiona ni sehemu ya utaratibu huo.
Hata hivyo viongozi
wa dini kwa nyakati tofauti wamesema kuwa wanaunga mkono serikali kufanya
mahafali hayo ya pamoja na utaratibu huo watahimiza kwa waumini wao kuweza
kuchangia katika elimu kwani ni sehumu ya urithi mzuri kwa jamii sanjari na
kuhimiza kujitolea kusaidia wanafuzni hao kuweza kujenga taifa lenya maadili.
Rc Gambo Ni Heri Arusha Kuwa wa Mwisho Kuliko Udanganyifu
Reviewed by KUSAGANEWS
on
October 31, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
October 31, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment