Kiongozi wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ametoa ushauri kwa
viongozi wenzake wa vyama vya upinzani kujiandaa kwa ajili ya kushiriki katika
chaguzi nyingine zote zinazofuata
Amewataka kujitathmini wakati wa kuelekea chaguzi ndogo
zijazo, uchaguzi wa serikali za Mitaa mwaka ujao na Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020
Zitto ambaye ni Mbunge wa Kigoma Mjini amebaini kwamba
wanasiasa wa upinzani wakiwamo wabunge na madiwani kukimbilia CCM kwa sababu
yoyote ile ni vita ya Kisaikolojia inayolenga kuwakatisha tamaa wanachama wa
vyama vya upinzani, wafuasi na wananchi
Ameandika wasikubali kuingizwa katika vita hiyo.
Zitto ametoa kauli hiyo leo Agosti 14 kupitia ukurasa wake
wa Twita.
CCM imeshinda katika
kata zote pamoja na jimbo hilo kupitia mgombea wake, Christopher Chiza
“Baada ya kugomea chaguzi za Songea Mjini na Singinda
Kaskazini, ni dhahiri hatupaswi kugomea chaguzi nyingine yeyote. Ushirikiano
madhubuti wa vyama vya upinzani (kimkakati) na wapenzi wa demokrasia
unahitajika zaidi wakati huu kuliko wakati mwingine wowote. Kwa mfano kuwe na
watazamaji wa ndani kwa kila chaguzi ili waweze kukusanya kila taarifa za
ukiukwaji wa sheria au kanuni za uchaguzi,”ameandika Zitto
Katika ufafanuzi wa hoja yake, Zitto amesema miezi michache
ijayo mashambulizi dhidi ya vyama vya upinzani na wanaharakati wa haki za
binadamu na haki za demokrasia yataongezeka zaidi
“Wale tu wenye dhamira ya dhati ya kujenga Tanzania yenye
Maendeleo ndani ya Demokrasia ndiyo watabaki na tutashinda hatimaye.”ameandika
Zitto asema wapinzani kukimbilia CCM ni vita ya kisaikolojia
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 14, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment