Wanawake wawili wanashikiliwa na polisi mkoani Morogoro kwa
tuhuma mbalimbali akiwamo mmoja aliyemuua mtoto wake wa kiume wa miaka 11 kwa
kumpiga fimbo kichwani
Katika tukio jingine mwanamke mwingine anashikiliwa na
polisi akituhumiwa kumsokomeza mwiko sehemu za siri mtoto wa dada yake mwenye
umri wa miaka sita
Kamanda wa polisi mkoani Morogoro, Wilbroad Mutafungwa
amesema hayo leo Agosti 14 wakati akitoa taarifa ya matukio mbalimbali ya
mkoani humo kwa waandishi wa habari
Kamanda Mutafungwa amesema matukio yote yametokea katika
wilaya za Gairo na Manispaa ya Morogoro na kwamba watuhumiwa wote watafikishwa
mahakamani mara moja.
Mama mbaroni kwa kumuua mtoto wake kwa fimbo
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 14, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment