Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka viongozi wa vyama vya
ushirika wawatumikie wanachama wao ipasavyo na wasidhani hiyo ni sehemu ya
kupiga dili
Amesema Serikali itawachukulia hatua kali viongozi wote wa
vyama vya ushirika watakaobainika kuhujumu wana ushirika, hivyo amewataka wafanye
kazi kwa uaminifu
Ametoa kauli hiyo jana Alhamisi, Agosti 16, 2018 wakati
akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kijiji cha
Chomachankola, mkoani Tabora
Amewataka viongozi wa chama Kikuu cha Ushirika cha Mkoa wa
Tabora cha Igembensabo kuhakikisha wanasaidia wakulima kujiunga na huduma ya
bima ya afya
Amesema tayari mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF)
umeanzisha huduma kwa ajili ya wanachama wa vyama vya ushirika ambao wanatakiwa
kuchangia Sh75,000 kwa mwaka
Waziri Mkuu amesema wanachama hao wakijiunga na mfuko huo
watapata fursa ya kutibiwa bure wao, wenza wao na watoto wanne kwenye hospitali
mbalimbali nchini ikiwemo ya Taifa Muhimbili
Pia amewahamasisha wananchi wa wilaya hiyo wajiunge na Mfuko
wa Afya wa Jamii (CHF) ili waweze kuwa na uhakika wa kupata matibabu wao pamoja
na familia zao kwenye hospitali zilizoko ndani ya mkoa Tabora
Katika hatua nyingine, Majaliwa amewataka wakulima wa zao la
pamba wajiandae kwa kupanua mashamba yao katika msimu ujao wa kilimo kutokana
na uwepo ya masoko ya uhakika
Amesema kwa sasa kuna viwanda vingi vya kuchambua pamba
ambavyo vimeanza uzalishaji na baadhi ya wamiliki wake wamelalamikia upungufu
wa malighafi
Waziri Mkuu asema ushirika si pa kupigia dili
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 17, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment