Mkuu wa Wilaya ya Longido ambaye pia ni mwenyekiti wa
kamati ya Ulinzi na Usalama Frank Mwaisumbe amemaliza mgogoro uliyokuwepo kati ya Kampuni ya Uchimbaji Madini ya Sendeu Inverstment LTD na Mundarara Group Mining iliyopo
eneo la Mundarara eneo ambalo ni maarufu kwa auchimbaji wa madini ya Ruby ambao umedumu kwa muda mrefu bila Maelewano.
Akizungumza na Kusaga News Ofisini Kwake Mkuu Huyo Bwana
Mwaisumbe amesema kuwa baada ya agizo la waziri wa madini Mh Angela Kairuki aliagiza
mgogoro huo ufanyiwe kazi na Ashughulikiwe mara moja ili shughuli
za uchimbaji ziendelee
Mwaisumbe Amesema kuwa baada ya agizo hilo aliunda
kamati ya Uchunguzi kwa ajili ya kushughulikia mgogoro wa kampuni hizo mbili za
uchimbaji wa madini na hatimaye leo Agost 17 ,2018 amekutana na pande zote
mbili na kutoa maagizo ambayo watayatekeleza ili kumaliza Mgogoro huo wa
wachimbaji wa migodi hiyo.
Ameongeza kuwa katika kikao hicho cha usuluhishi wa
pande mbili kama serikali wametoa maagizo kumi ambayo yote yamekubaliwa kwa
ajili ya kufanyiwa kazi na kuahidi ushirikiano baina yao kama wawezekazaji
kwasababu serikali bado inahitaji wawekezaji ili kupata maendeleo zaidi.
Hata hivyo ametoa wito kwa wamiliki wa madini kutumia
nga\zi hudika katika kutatua migogoro kwakua hapo awali walikuwa wanawatumia
watu ambao hawahusiki kama wanasiasa wasaatu ambao hawawezi kuwasaidia huku
akiwataka wawezaji kujitokeza kushirikiana na serikali kwasababu maeneo ya
uwekezaji bado yapo na vibali vinapatikana.
Kwa upande wa Mkurugenzi wa kampuni ya Sendeu
Inverstment Ltd Gabriel Sendeu Laizer ambaye walikuwa na Mgogoro na Kampuni ya
Sendeu Mining amemshukuru Mkuu wa Wilaya Mh Mwaisumbe kwa kumaliza mvutano
uliyokuwepo kwasababu ulikuwa unaikosesha pia serikali mapato stahiki na
kuahidi kushughulikia yote walioagizwa kuyafanya.
Sendeu amesema kuwa kinachofanyika kwasasa ni kufanya
vipimo ambavyo vitasaidia wao kutoingiliana katika mipaka ambayo inatenganisha
Maeneo ya wawekezaji hao wawili ambapo wao walitoboa upande wa kampuni ya
Sendeu mining.
Naye Muwekezaji wa kampuni ya Mundarara Miningi amesema
kuwa mgogoro huo umemalizika kwa amani na wataendelea kushirikiana kwa pamoja kwasababu
mgogoro huo ulisababisha kupunguza mapato ya kijiji kwa zaidi ya asilimia 90.
DC Mpya Longido awaweka kati wawekezaji wa Madini waliokuwa na Mgogoro wa Muda mrefu
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 17, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment