Waziri Mbarawa azindua dira ya maji ya malipo kabla


Waziri wa Maji na Umwagiliaji Professa Makame Mbarawa amezindua Dira ya maji ya malipo kabla (prepaid meter) jijini Mwanza leo Agosti 15 na kuwataka watendaji wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira (Mwauwasa) kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa huduma hiyo

Amezindua huduma hiyo kwa kufunga mita hiyo nyumbani kwa mkuu wa wilaya ya Nyamagana Dk Philis Nyimbo akiwa ni mteja wa pili kufungiwa mita hiyo akitanguliwa na mkuu wa mkoa huo John Mongella

Amesema kuzindua mfumo huo ni jambo moja lakini hautakuwa na maana endapo wananchi wanaolengwa kama hawatapewa elimu jinsi ya kujiunga na kufahamu umuhimu wa matumizi yake.

 Ameagiza mamlaka hiyo kuzifungia kwanza taasisi za serikali, mahoteli na viwanda ambapo mfumo huo ukiunganishiwa wateja wengi utainua mapato yao

"Tumezindua mfumo huu leo, ni mzuri lakini tunapaswa kutoa elimu kwa wananchi ambao ndio wateja wetu ili wawe na uelewa, mkifanya hivyo ninaamini kuna mabadiliko makubwa yatapatikana," amesema

Meneja mifumo ya mawasiliano wa Mwauwasa, Alena Kalinjuna amesema kwa sasa mamlaka imeshanunua mita 117 za malipo kabla zenye ukubwa tofauti ambazo zitafungwa kwa awamu kwa wateja mbalimbali

Amesema miongoni mwa faida za mfumo huo ni pamoja na kuongeza mapato, kupunguza kiasi cha maji yanayopotea na kupunguza udanganyifu

Amesema kwa mwaka wa fedha 2019/20 wanalenga kuwafungia mita hizo wateja 500 wakianza na taasisi za serikali

Mkoa wa Mwanza una jumla ya wateja wa 75,629 wanaohudumiwa na Mwauwasa huku malengo yakiwa ni kufikisha wateja 100,000 ifikapo Juni 2019

Waziri Mbarawa azindua dira ya maji ya malipo kabla Waziri Mbarawa azindua dira ya maji ya malipo kabla Reviewed by KUSAGANEWS on August 15, 2018 Rating: 5

No comments: