Serikali yajadili kuadimika kwa Saruji


Serikali imekutana na wadau wa sekta ya viwanda kujadili kuadimika kwa saruji, huku inayopatikana ikiuzwa bei ya juu

Kikao hicho kinachoongozwa na Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Stella Manyanya kimehudhuriwa na wazalishaji wa saruji na wa makaa ya mawe, wasafirishaji na wadhibiti.

 Akizungumza katika mkutano huo unaofanyika jijini Dar es Salaam leo Agosti 15, 2018 Manyanya amewataka wazalishaji wa saruji kueleza uwezo wao wa uzalishaji

Naibu waziri pia amewataka kueleza sababu za kusimamisha uzalishaji ghafla na kwa viwanda vyote

"Imetushitua kuona saruji imepotea sokoni na kupanda bei ghafla, tena viwanda vyote. Tukasema hapo ni zaidi ya masuala ya kiufundi, kwa hiyo tumewaita kuwasikiliza tujue tatizo ni nini ikiwezekana leo tutoke na uamuzi,” amesema Manyanya

Naibu waziri amesema sasa kuna fursa nyingi za soko la saruji kupitia miradi inayotekelezwa na Serikali.

 Amesema hiki ndicho kipindi cha kuongeza uzalishaji lakini anashangazwa kuona saruji imeadimika na bei imepanda
Serikali yajadili kuadimika kwa Saruji Serikali yajadili kuadimika kwa Saruji Reviewed by KUSAGANEWS on August 15, 2018 Rating: 5

No comments: