Katika hali
isiyo ya kawaida waziri anayehusika na Masuala ya Wanawake nchini New Zealand
ametumia usafiri wa baiskeli kuelekea hospitali kwa ajili ya kujifungua
Waziri huyo
Julie Genter anayetoka chama cha Kijani alisema kwamba aliamua kutumia usafiri
huo kwa sababu gari lake halina nafasi ya kutosha
Kiongozi huyo
alipiga picha na mume wake wakielekea hospitali kwa kutumia usafiri huo wa
baikeli na kuiweka katika akaunti yake ya Instagram
Kuanzia mwezi
wa sita mwaka huu Mbunge, Jacinda Ardern na Genter walikua wakihudhuria kliniki
pamoja katika hospitali moja iliyopo mjini Auckland
Genter 38,
aliyejifungua mtoto wa kwanza aliandika katika mtandao wake wa Instagram,
''mtuombee, mimi na mwenzangu tumepanda kwenye baiskeli kwa sababu hakukua na
nafasi’’
Mbunge wa
kwanza kupata mtoto akitumikia bunge la New Zealand, ilikua mwaka 1970, huku
mwingine akinyonyesha kwa mara ya kwanza katika eneo la kazi mwaka 1983
Waziri atumia baiskeli kwenda hospitali kujifungua
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 20, 2018
Rating:
![Waziri atumia baiskeli kwenda hospitali kujifungua](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiM6ax-XP2Q8Y75NF5nvewEeet6dJ7XNsnOyeRYdwLGU1E7XCP5N74TmCxoGLSldg8T6mJk7-1k2Ht88gNb77_5BV6RBazLn8uFtKSOUb27_Bhav7gbNXtcMcYPA1mnObqXigajSJfcuZM/s72-c/4.jpg)
No comments:
Post a Comment