Serikali imekiri bado haina uwezo wa kuwazuia Watanzania
waliosomeshwa kwa fedha za Serikali kuajiriwa nchi nyingine licha ya uhaba wa
wataalamu wa mafuta na gesi kuwapo nchini
Akizungumza leo Agusti 20, 2018, Katibu Mkuu wa Wizara ya
Nishati, Dk Khamisi Mwinyimvua amesema kwa sasa Serikali haina utaratibu wa
kuwazuia Watanzania kufanya kazi kwenye kampuni zilizopo nje ya nchi
"Serikali imekuwa ikifanya jitihada za kutoa ufadhili
kwa wanafunzi na lengo ni kuongeza wataalamu ili kukidhi mahitaji, lakini ni
vigumu kumzuia mtu asiende kufanya kazi sehemu nyingine," amesema
Mwinyimvua wakati wa hafla ya kuwaaga wanafunzi 20 watakaokwenda nchini China
kusoma mwaka huu
Amesema jumla ya watanzania 100 wamepelekwa China kwa
ajili mafunzo maalumu kwenye sekta ya mafuta na gesi huku changamoto ikiwa ni
jinsi gani nchi inanufaika na wataalamu hao
Amesema kwa kiasi kikubwa kazi za uvunaji mafuta na gesi
zinaendeshwa na kampuni binafsi hivyo inashindwa kutoa nafasi nyingi za ajira
kwa wazawa
Hata hivyo, amesema kupitia sheria ya ajira imeweka
msisitizo kwa kampuni za kugeni kuajiri Watanzania wengi ili kunufaika na
rasilimali za ndani
"Ni fedha nyingi zinapotea kwa kukosa wataalamu kwa
sababu Watanzania sio wengi kwenye sekta hii," amesema
Aidha amesema kupitia mpango wa kuwasomesha watu nje ya
nchi, kutasaidia kutatua changamoto ya uhaba wa wataalamu hususan kwenye mafuta
na gesi
Naye Naibu balozi wa China,XU Chen amewahimiza wanafunzi hao
kuwa wazalendo kwa nchi yao hasa katika kukuza sekta ya gesi ambayo ina mchango
mkubwa kwa uchumi wa Taifa
"Tanzania ina utajiri mkubwa wa rasilimali ila bado
mnahitaji wataalamu ambao wanaweza kuzalisha kwa maendeleo ya nchi,"
amesema
Kwa upande wake, Emmanuel Kessy ambaye ni mmoja wa wanafunzi
wa shahada ya uzamivu aliahidi kuwa wapo tayari kuitumikia nchi yao kwa weledi
mara baada ya kurejea nchini
"Sisi tunakwenda kufanya kazi kwelikweli kwa sababu
nchi imetutuma na tukirudi tutatafuta jinsi gani ya kuifanya gesi kuwa biashara
yenye manufaa zaidi," amesema
Mpango huo unafanyika chini ya mkataba wa miaka saba kati ya
China na Tanzania ulioanza mwaka 2013 ambapo hadi sasa jumla ya watanzania 100
wamenufaika na mafunzo hayo
Serikali yatoa neno Watanzania kuajiriwa nje ya nchi
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 20, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment