Wanamuziki
ambao nchini Uganda wameshindwa kuzuia machozi yao baada ya kufika nyumbani kwa
Mbunge Bobi Winne
Wanamuziki hao
wakikiwakilisha Chama cha wanamuziki nchini nchini humo (UMA) kimepeleka msaada
kwenye familia ya Winne anayeshikiliwa katika gereza la Makindye kwa
madai ya kushambulia msafara wa Rais Yoweri Museveni
Wanamuziki hao
walifika nyumbani eneo la Magere anapoishi mwanamuziki huyo na kumkuta
mke wake Barbra Kyagulanyi na kumkabidhi msaada ikiwamo chakula
Mke wa Bobi
Wine aliwaeleza wanamuziki hao kwa masikitiko kwamba mume wake anapata tabu
sana kwa kuugulia maumivu yaliyotokana na kupigwa na wanajeshi
Kyagulanyi
alisema kwenye waraka wake kwamba alifanikiwa kumuona mume wake akiwa
katika gereza la jeshi la Makindye akiwa katika hali mbaya
Alisema
kwamba alifika gerezani hapo akiwa na watu wa haki za
binadamu,mwanasheria wake na akamuona mume wake huyo akiwa hai licha ya kuwa na
hali mbaya hivyo anamuomba Mungu amsaidie apone
''Bobi
ameumizwa, anamaumivu makali kila sehemu anatia huruma tumuombeeni hawezi
kusimama wala kutembea''alisema
Alisema mume
wake anaongea kwa tabu sana,anatoa damu puani anahitaji kupatiwa huduma za
kipekee chini ya uangalizi wa daktari wake
Mwanamuziki
maarufu Ronald Mayinja wako pamoja na Familia ya mwanamuziki huyo
na kwamba wanatimiza wajibu wao kama ndugu wengine walioguswa na tatizo ambalo
limemkuta mwenzao
Baadhi ya
wanamuziki maarufu ambao walifika nyumbani kwa Bobi Wine ni pamoja na
Juliana Kanyomozi, Moureen Nantume, Haruuna Mubiru, Spicy Diana, Litto Boss,
Rema Namakula, Evelyne Lagu na Winnie Nwagi.
Mke wa Bobi Winne awatoa machozi wanamuziki waliomtembelea
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 20, 2018
Rating:
![Mke wa Bobi Winne awatoa machozi wanamuziki waliomtembelea](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg2mGk4ExKjmVzLK3H63kArqnGUnPzr9ODuSi-xayjPulbweNueQ_VqOJRugEifylqNiY698PjW_b7K2Yhcn8BQ9ouTVsbm6qk1azY1gT9XA1h-FVXJpmO0SJTVQIKkyV93pJ1hiFbB8YA/s72-c/_102724617_f3a6e0af-b193-49f8-8120-a541cbec159a.jpg)
No comments:
Post a Comment