Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto, Dk Faustine Ndugulile amepiga marufuku uuzwaji wa vifaa vya kupimia
virusi vya Ukimwi kwa watu binafsi
Naibu waziri huyo amesema hatua hiyo inatokana na sheria za
nchi kutoruhusu mtu kujipima mwenyewe
Hayo ameyasema leo Agosti 20, 2018 katika hafla ya
kukabidhiwa cheti cha ubora wa kimataifa (ISO) kwa Mfuko wa Taifa wa Bima ya
Afya (NHIF).
Ndugulile amesema kwa mujibu wa sheria iliyopo sasa
inaruhusu mtu kupimwa virusi vya Ukimwi na mtaalamu au mtoa huduma kutoka kituo
cha afya na si vinginevyo
"Hivi sasa bado tuko katika hatua ya kubadilisha sheria
ili tuweze kuruhusu watu kujipima wenyewe lakini hii itakuwa baada ya majaribio
yanayofanyika katika baadhi ya maeneo kuonyesha matokeo chanya," amesema
Ndugulile
"Kwa hiyo basi naziagiza taasisi zangu kuhakikisha kuwa
zinadhibiti uuzwaji holela wa vifaa hivi katika maduka ya dawa kote
nchini," ameongeza
Ndugulile apiga ‘stop’ uuzwaji vifaa vya kupimia Ukimwi
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 20, 2018
Rating:
![Ndugulile apiga ‘stop’ uuzwaji vifaa vya kupimia Ukimwi](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEirDasAUz2TJjPtxsy5JsjO2-CH3_qFXMT55eOfC3RCyFuQ_G9KUNMVECtrK3stXauOAhtZEgblO41p47P3k7wMIDYFJptqTjyadck0JOQbujJF4Y63q4eNI8M16zb60fUDrcVTVdlZAz0/s72-c/_102724617_f3a6e0af-b193-49f8-8120-a541cbec159a.jpg)
No comments:
Post a Comment