MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema mfumo wa
anwani za makazi na mwongozo wa postikodi ukikamilika utasaidia kudhibiti wezi
na matapeli katika Jiji la Dar es Salaam
Amesema pia utarahisisha huduma na kumwezesha kila mwananchi
kuwa na anwani, kuwasaidia wageni kujua maeneo, kulisaidia Jeshi la Zimamoto na
Ukoaji kufika haraka kwenye eneo lenye tukio
Aliyasema hayo kwenye ufunguzi wa warsha kwa viongozi wakuu
wa Mkoa wa Dar es Salaam iliyohusu ukusanyaji wa taarifa za anwani za makazi na
wanakaya, iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA
"Mfumo huu ni ukombozi kwa wananchi wa Jiji la Dar es
Salaam kwa kuwa utarahisisha huduma na kuwezesha kila mwananchi kuwa na anwani
"Pia utasaidia Jiji la Dar es Salaam kuwa katika
mpangilio wa kisasa na kuhakikisha mitaa yote inawekwa katika mfumo wa anwani
za makazi na postikodi," alisema Makonda
Alieleza kuwa mfumo huo utasaidia kuwaunganisha wananchi wa
Jiji la Dar es Salaam kwa kuwa utakuwa katika mpangilio wa kisasa
Alisema mpango huo utawasaidia wageni wanaoingia katika jiji
hilo kutokutapeliwa wanapotumia vyombo vya usafiri kufika maeneo wanayokwenda
"Abiria mgeni akishuka uwanja wa ndege au kituo cha
mabasi cha Ubungo itakuwa rahisi kwake kutoa kiwango sahihi cha pesa huko
aendako kwa sababu atakuwa anafahamu umbali na sehemu aendako," alisema
Makonda
Aidha, aliwaomba TCRA kupeleka elimu hiyo kwa madiwani na
wenyeviti wa mitaa ili kuwajengea uelewa
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Connie Francis, alisema
utaratibu wa kukusanya taarifa za anwani za makazi umeboreshwa na kwa sasa
taarifa hizo zitachukuliwa kwa kutumia mfumo wa kielektroniki(e-PRS
Alisema mfumo huo utasaidia wananchi kujitambulisha
anapoishi na kupatiwa huduma kwa urahisi, kuboresha huduma za uokoaji na za
dharura, kurahisisha huduma za misaada inapotokea maafa, kufikisha mizigo
nyumbani na ofisini
"TCRA inatambua kuwa jukumu la kutoa majina ya mitaa na
barabara na kuweka namba za nyumba kisheria ni la mamlaka za Serikali za Mitaa,
lakini kwa kuzingatia umuhimu wa kuboresha utoaji na ufikishaji wa huduma za
mawasiliano kwa jamii, TCRA ilisimamia utekelezaji wa mpango huu katika awamu
ya majaribio," alisema Francis
Alisema utekelezaji wa awali ulifanyika katika baadhi ya
kata za majiji zikiwamo kata nane za Jiji la Arusha, nane za Jiji la Dodoma na
45 kwa Jiji la Dar es Salaam, ambalo umefanyika kwa awamu tatu; ya kwanza
zilikuwa kata 32, awamu ya pili 13 na awamu ya tatu utekelezaji wake
unakamilishwa hivi karibuni
Makonda Kuja na Mkakati wa Kuthibiti Wezi na Matapeli
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 20, 2018
Rating:
![Makonda Kuja na Mkakati wa Kuthibiti Wezi na Matapeli](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhF22mti2p6XIIIw7B9jVfXbTiBNZXeuYHhGtW1F1LWgLrZKizeZRfFwTBpbg94Tsfq4qtYQNxjcz_q0LIIvyygMsU9Pu6PnHdAEjCDLttjj2O_NDoh8P9RoZjdCAYiCBSXIXiMxPG70bM/s72-c/_102724617_f3a6e0af-b193-49f8-8120-a541cbec159a.jpg)
No comments:
Post a Comment