Afungwa Jela Milele kwa Kulawiti Mtoto


MAHAKAMA ya Wilaya ya Lindi imemuhukumu Mussa Milanzi (29), kifungo cha maisha baada ya kupatikana na hatia ya kumlawiti mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka mitano

Hakimu wa mahakama hiyo Erasto Phili, alitoa hukumu hiyo baada ya kuridhika na ushahidi wa kitaalamu wa idara ya afya na upande wa mashtaka

Kabla ya hukumu hiyo mshtakiwa huyo alitoroka baada ya kupewa dhamana na kwenda kujificha Wilaya ya Masasi, mkoani Mtwara, ambako alikamatwa na kurejeshwa mkoani Lindi

Awali Mwanasheria wa Serikali, Yahaya Gumbo aliiambia mahakama hiyo kwamba Oktoba 11, mwaka jana mchana, mshtakiwa akiwa kwenye kazi yake ya kuchunga ng'ombe eneo la pori la Angaza, Manispaa ya Lindi, watoto walikuwa wakimfuata nyuma na mifugo yake ndipo alipomkamata mmoja wao na kumlawiti

Mshtakiwa huyo alipotakiwa kujitetea, aliiomba mahakama imuonee huruma kwa kuwa ana mke na mtoto mchanga na kwamba akipewa adhabu hiyo watakosa huduma yake

Alidai kuwa alifanya kitendo hicho kutokana na kupitiwa na upepo mbaya

Baada ya utetezi huo, Mwanasheria wa Serikali Yahaya Gumbo, aliiomba mahakama kumpa mshtakiwa huyo adhabu kali ili iwe fundisho kwake na wengine wenye tabia kama hiyo, ikizingatiwa amefanya unyama huo kwa mtoto asiye elewa kitu chochote

Hakimu Phili akitoa hukumu hiyo alisema licha ya utetezi huo, kitendo cha kinyama alichomfanyia mtoto huyo asiye na hatia hakiwezi kuachiwa kiendelee

Afungwa Jela Milele kwa Kulawiti Mtoto Afungwa Jela Milele kwa Kulawiti Mtoto Reviewed by KUSAGANEWS on August 20, 2018 Rating: 5

No comments: