Wanaotumia Watoto Migodini Kukiona Cha moto


SERIKALI Wilayani Kahama mkoani Shinyanga imesema itawachukulia hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kuwafikisha mahakamani wanaowatumia watoto wadogo chini ya miaka kumi na nane katika shughuli za uchimbaji wa madini

Watoto wadogo wamekuwa wakitumiwa na wachimbaji wadogo wa madini hasa katika shughuli za kuchota maji na kusomba mawe ya dhahabu na kupeleka katika maeneo ya uchenjuaji wa madini, hali ambayo inawafanya watoto hao kukosa masomo

Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Anamringi Macha, alisema jana lengo la serikali ni kuona kila mtoto mwenye umri wa kwenda shule anakwenda shuleni kupata elimu ambayo itakuwa mkombozi kwa maisha yake ya baadae

Alisema asilimia kubwa ya wananchi  wilayani hapa wanajishughulisha na uchimbaji wa madini, kilimo na ufugaji, hali hiyo ndio inayopelekea watoto kukosa masomo na kuinguia katika shughuli hizo

"Nataka kuona kila mtoto mwenye umri wa kwenda shule anakwenda shuleni mara moja na sio kwenda katika shughuli za uchimbaji wa madini, kilimo au kwenda kuchunga mifugo ya baba yake,” alisema

Macha aliongeza: “Tunataka kuona wazazi wanakuwa mstari wa mbele kulitokomeza hili la watoto kutumikishwa na wachimbaji wadogo na kwahili lazima tushirikiane na wazazi, viongozi wa wachimbaji na wachimbaji wenyewe

Alisema mambo mengi yanatokana na wazazi kuwa na mwamko mdogo wa elimu hasa wale waliko pembezoni mwa mji na kwamba serikali itaendelea uwapatia elimu ili watambue umuhimu wa elimu kwa watoto wao

Katika hatua nyingine  Macha alisema kila mfanyabiashara ambaye anafanya biashara inayomwingizia kipato anatakiwa kulipa kodi kwa wakati sambamba na kutumia vema mashine ya elektroniki (EFD) ili kupunguza migogoro yao na Mamkala ya Mapato (TRA

Alimtaka Meneja wa TRA mkoa Mkoa maalum wa kikodi Kahama, Jacobo Mtamang'ombe, kutoa elimu juu ya matumizi ya EDF kwa wafanyabiashara walioko pembezoni mwa mji

Wanaotumia Watoto Migodini Kukiona Cha moto Wanaotumia Watoto Migodini Kukiona Cha moto Reviewed by KUSAGANEWS on August 20, 2018 Rating: 5

No comments: