TAASISI ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika, Tawi la
Tanzania (Misa-Tan), imesema inasikitishwa na vitendo vya ukiukwaji wa haki za
binadamu na unyanyasaji kwa waandishi wa habari unaoendelea nchini wakati
wakitekeleza wajibu wao wa kuhabarisha umma
Aidha, MISA Tanzania inapinga vikali vitendo hivyo viovu na
ukandamizwaji wa wanahabari na haki za kupata habari, huku ikiwataka wenye
mamlaka kuomba radhi na kuchukua hatua stahiki kwa waliotenda vitendo hivyo
vinavyochafua Jeshi la Polisi nchini
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari
na Misa–Tan nakusainiwa na Mwenyekiti wake Salome Kitomari, kwa sasa kuna
tishio la unyanyasaji wa waandishi wa habari na watetezi wa haki za binadamu
kunakofanywa na vyombo vya dola
"Uhuru wa vyombo vya habari ni haki ya msingi
inayotamkwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 18,
ambayo imetokana na tamko la haki za binadamu la Baraza la Usalama la Umoja wa
Mataifa na kupewa nguvu ya kisheria kwa tamko la pamoja la nchi za Afrika ya
haki za watu na haki za binadamu," ilisema sehemu ya taarifa hiyo
Alisema MISA Tanzania inasikitishwa na vitendo vya hivi
karibuni vya ukiukwaji wa haki za binadamu na unyanyasaji kwa waandishi wa
habari unaoendelea nchini wakati wakitekeleza wajibu wao wa kuhabarisha umma
"Tunaungana na wadau wote wa habari na watetezi wa haki
za binadamu kupinga vikali vitendo vya kiudhalilishaji kwa mwandishi wa habari
za michezo wa Wapo radio, Sillas Mbisse, kwa kupigwa na polisi akiwa chini ya
ulinzi wa polisi hao wakati akitekeleza wajibu wake wa kukusanya habari katika
Uwanja wa Taifa Agosti 8, mwaka huu jijini Dar es Salaam,” alisema Kitomari
Alisema, tukio hilo la kufedhehesha na kusikitisha lilitokea
Siku ya Simba Day wakati klabu maarufu nchini Simba Sports Club huadhimisha kwa
kutambulisha wachezaji na siku hiyo walicheza mchezo wa kirafiki na timu ya
Asante Kotoko ya Ghana
Michezo huwakusanya watu pamoja bila kujali rangi zao,
itikadi, historia, dini, imani na hadhi ya mtu. Ni maajabu sana kwa mwanahabari
kupigwa na polisi mbele ya watu na siyo mashabiki wa timu bali na watu wenye
jukumu la kulinda usalama wa raia na mali zao," Mwenyekiti huyo alisema
pia kwa kauli moja, MISA Tanzania inaungana na wadau wengine kupinga kitendo
cha kupigwa na kunyanyaswa kwa mwandishi wa habari wa Tanzania Daima, Sitta
Tuma, katika kata ya Turwa, Wilaya ya Tarime, Mkoa wa Mara.
Alisema mwandishi huyo alikamatwa na kisha kupigwa na polisi
wakati akikusanya habari za uchaguzi na ukiukwaji wa sheria za uchaguzi
wilayani humo
"Vitendo hivi si tu kwamba vinaondoa uhusiano mzuri wa
utendaji kazi kati ya polisi na wanahabari, lakini vinawanyima haki wanahabari
kukusanya habari na raia kupewa taarifa iliyokamilika," alibainisha
Kitomari
Alisema waandishi wa habari wanafanya kazi ili kuhakikisha
kuwa haki hiyo inakuwapo ili kujenga demokrasia na kulinda utawala wa sheria
Misa-Tan Yalaani wanahabari Kunyanyaswa.
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 20, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment