Abiria 60 wanusurika kifo baada ya basi walilokuwa
wakisafiria kutoka Kigoma kwenda Sumbawanga mkoani Rukwa kuteketea kwa moto
Akizungumza kwa njia ya simu kamanda wa polisi mkoani Kigoma
Martin Ottieno amesema tukio hilo limetokea leo Agosti 20 eneo la Kazurambimba
wilayani Kigoma
Kamanda Ottieno amesema kwamba basi lililopata ajali hiyo
linamilikiwa na Kampuni Saratoga.
"Hakuna abiria aliyepoteza maisha wala kupata madhara
ya aina yoyote zaidi ya baadhi ya mizigo yao kuteketea kwa moto," amesema
Kamanda Ottieno
Polisi wanaendelea kuchunguza chanzo cha ajali hiyo
Abiria 60 wanusurika basi likiteketea moto Kigoma
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 20, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment