WALIMU 24 wamepelekwa katika Shule ya Sekondari ya Jangwani
kuziba nafasi za walimu walioondolewa shuleni hapo kutokana na matokeo mabaya
iliyoyapata kwenye mtihani wa kidato cha sita, mwaka huu.
Ofisa Elimu Mkoa wa Dar es Salaam, Hamis Lissu, aliiambia
Nipashe kuwa tayari serikali imejipanga kuinua kiwango cha taaluma shuleni hapo
kwa kupeleka walimu wapya baada ya kuwaondoa waliokuwapo
Alisema tayari wameondoa walimu 48 na wamepeleka walimu
wapya 24 ambao wamewatoa wilaya zote za Jiji la Dar es Salaam.
Tumeshaanza kupeleka walimu katika Shule ya Jangwani, lakini
pia baadhi yao tumewaondoa. Kazi hii ya kutoa na kupeleka walimu inafanywa kwa
umakini na utaalamu mkubwa, hatukurupuki. Tunataka kuhakikisha wanaopelekwa ni
walimu wazuri," alisema Lissu.
Alibainisha kuwa jumla ya walimu waliokuwapo katika shule
hiyo ni 87, lakini ina 63 baada ya baadhi yao kuhamishwa.
Bado tunaendelea kuiimarisha shule hiyo katika maeneo yote,
mbali na kuweka nguvu kwa walimu, tumepanga kuimarisha pia usimamizi wa nidhamu
kuanzia kwa wanafunzi wenyewe mpaka juu na tunaimarisha ulinzi pia," Lissu
alisema.
Agizo la kubadilisha uongozi na walimu wa shule hiyo
lilitolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali
za Mitaa (Tamisemi), Seleman Jafo, baada ya shule hiyo kuwa miongoni mwa shule
10 zilizofanya vibaya zaidi katika matokeo ya mtihani wa kidato cha sita
yaliyotolewa Julai 13, mwaka huu.
Katika agizo lake, Jafo pia alitaka kuondolewa kwa walimu
waliokaa muda mrefu shuleni hapo, akiongeza kuwa shule hiyo ilikuwa na sifa
kubwa kitaifa na ilikuwa ni ndoto ya kila msichana kusoma hapo.
Katika matokeo hayo, shule hiyo ilishika nafasi ya 451 kati
ya 453 zilizofanya mtihani huo
Walimu 24 wapelekwa Jangwani Shule iliyofanya Vibaya
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 16, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment