ALIYEKUWA msaidizi wa mgombea udiwani wa Kata ya Kaloleni
kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Ibrahim Issa
(32), amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Arusha akiwa na majeraha
yake, kwa tuhuma za kumjeruhi Idd Musa
Akisoma hati ya mashtaka Wakili wa Serikali, Mary Lucas alidai
mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Chrisanta Chitanda, alidai
mtuhumiwa huyo alimjeruhi Iddi Mussa Agosti 12, mwaka huu, katika eneo la
Kaloleni
Alidai kuwa siku ya tukio mtuhumiwa alimjeruhi kwa kumchoma
kisu mkono wa kushoto Musa na kumsababishia jeraha.
Wakili huyo aliiomba mahakama hiyo kuahirisha kesi hiyo na
kuipangia tarehe nyingine kutokana na upelelezi wake kutokukamilika
Hata hivyo, mshtakiwa huyo alikana kutenda kosa hilo
Mtuhumiwa anayetetewa hapo na Wakili SheckMfinanga,
aliachiwa baada ya kudhaminiwa na watu wawili ambao kila mmoja alitia
saini hati ya dhamana ya thamani ya Sh. milioni mbili
Hakimu Chitanda aliahirisha kesi hiyo hadi Septemba 17 mwaka
huu itakapitajwa tena
Agosti 12 majira ya saa nne asubuhi katika Kata
ya Kaloleni, vyombo vya habari viliripoti msaidizi wa mgombea
udiwani, Ibrahimu Issa, alijeruhiwa kwa kuchomwa kisu jicho la kushoto
na sehemu mbalimbali za mwili wake na kupelekwa katika Hospitali ya Rufani
ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru, ambako aliondolewa na kushikiliwa na
Jeshi la Polisi hadi jana alipofikishwa mahakamani
Mtuhumiwa afikishwa mahakamani Akiwa na majeraha yake
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 16, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment