Siku moja baada ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila,
kuliagiza Jeshi la Polisi kuwakamata na kuwaweka ndani wananchi wote wa Kijiji
cha Ngole, utekelezaji wa agizo hilo umeanza na tayari polisi wametinga
kijijini huko
Akizungumza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ulrich Mateo,
amesema magari kadhaa yametumwa yakiwa na askari wa kutosha kwa ajili ya
kuwakamata wananchi hao
Amesema kitendo kilichofanywa na wananchi wa kijiji hicho ni
uhujumu uchumi, hivyo ni lazima washughulikiwe ipasavyo.
Amesema baada ya agizo la Mkuu wa Mkoa, jeshi hilo lilipata
ushirikiano wa kutosha kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, William Ntinika
Polisi Watinga Kijijini cha Ngole Kukamata Wananchi Baada ya Agizo la Rc
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 16, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment