Siku moja baada ya kukemea tabia ya baadhi ya wakuu wa
wilaya kutumia vibaya mamlaka waliyonayo na kuwaweka watu ndani, Waziri wa
Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani
Jafo amewageukia wakurugenzi watendaji wa halmashauri.
Amewataka wakurugenzi
wapya kuepuka kujiingiza katika ugomvi wa kisiasa utakaokuwa chanzo cha
kushindwa kutekeleza majukumu yao ya kazi
Jafo akizungumza na wakurugenzi watendaji wapya wa
halmashauri jijini Dodoma jana, aliwataka kuepuka kujiingiza katika makundi ya
kisiasa na ugomvi usioeleweka ambao utawafanya kushindwa kutekeleza majukumu
yao
Wakurugenzi hao jana walikula kiapo cha ahadi ya uadilifu
kwa watumishi wa umma
“Simamieni mipaka yenu ya kazi, kila mtu akisimamia mipaka
yake kutakuwa hakuna migongano. Ninyi mnaenda huko kwa ajili ya utekelezaji wa
ilani ya CCM na hakuna mjadala mwingine,” alisema
Waziri Jafo alisema, “Msiende kujiingiza katika makundi ya
kisiasa na magomvi yasiyoeleweka inawezekana huko mnakokwenda kuna makundi ya
kisiasa yanayogombana. Inawezekana huko mnakoenda kuna watu wanagombana
simamieni ilani
“Leo hii unaenda katika halmashauri unamkuta mkurugenzi
kivyake, mwenyekiti wa halmashauri kivyake, mbunge kivyake, wakuu wa wilaya
kivyao.”
Alisema jambo hilo linafanya halmashauri nayo kwenda
kivyake, hivyo utekelezaji wa ilani kuwa mgumu. Alisisitiza uhusiano mwema
kazini na ushirikiano akisema, “Kuna baadhi ya watumishi wewe umefika pale ni
mgeni, mtu mwingine anakupiga dozi ya sumu iliyokolea hata wengine huwajui kwa
sura unaanza kuwachukia.”
Aliwaagiza kutenda haki kwa watu wote na kusimamia miradi ya
maendeleo, ukusanyaji wa mapato na kuhakikisha hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu
wa Hesabu za Serikali (CAG) zinajibiwa kwa wakati
Juzi, Jafo alikemea tabia ya baadhi ya wakuu wa wilaya
kutumia vibaya mamlaka waliyonayo na kuwaweka watu ndani, akisema inasababisha
wananchi kuichukia Serikali
Akizungumza wakati wa kikao kazi na wakuu wa wilaya 27
walioteuliwa hivi karibuni kilicholenga kuwapa maelekezo, aliwataka kuhakikisha
wanasoma na kuzielewa sheria zinazowaongoza ili kufanya kazi kwa weledi.
“Msiende kuwa vyanzo vya migogoro kwenye wilaya zenu, tumekuwa tukishuhudia
migogoro baina ya wakuu wa wilaya, wakurugenzi, wenyeviti wa halmashauri,
makatibu tawala na wabunge. Hatuwezi kwenda hivi, katengenezeni Serikali,”
alisema Waziri Jafo
Ujumbe wa katibu mkuu Jafo akisema hayo, Katibu Mkuu wa
Tamisemi, Mussa Iyombe aliwataka wakurugenzi hao kuhakikisha wanatenga muda wa
kuzungumza na watumishi badala ya kuwaachia maofisa utumishi ambao wamekuwa
wajeuri
“Tunapata tabu sana, mkurugenzi haingii ofisini. Ukimtafuta
humpati sasa wewe umepewa halmashauri halafu unatafutwa na waziri hupatikani,
unatafutwa na katibu mkuu hupatikani, unafanya kazi gani sasa?” alihoji
“Katika muda wote niliokaa hapa, wakurugenzi hawana urafiki
na watumishi. Wanaishia kwa maofisa utumishi, maofisa utumishi wajeuri
kwelikweli wanawaharibia sifa lazima mkawaangalie.”
Alisema hali hiyo imewafanya watumishi kusafiri safari ndefu
kwenda kumuona waziri wa Tamisemi wakati shida zao zingeweza kumalizwa na
mkurugenzi
Baada ya ma-DC Jafo awageukia ma-DED
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 16, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment