Wabunge kujadili ripoti ya CAG


TAARIFA ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha unaoishia Juni 30, mwaka jana, inatarajia kuchambuliwa kwenye vikao vya Kamati za Bunge zinavyotarajia kuanza keshokutwa

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Kitengo cha Habari, Elimu kwa Umma na Mawasiliano Ofisi ya Bunge, miongoni mwa mambo yatakayochambuliwa ni pamoja na taarifa hiyo ya CAG

Vikao hivyo vinatarajia kufanyika jijini Dodoma kabla ya kuanza kwa mkutano wa 12 wa Bunge uliopangwa kuanza Septemba 4, baada ya Spika wa Bunge, Job Ndugai, kuziita Kamati hizo kuanza shughuli zake

Taarifa hiyo ilieleza kuwa taarifa ya CAG itachambuliwa na kamati zinazosimamia matumizi ya fedha za umma ambazo ni Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) na Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC

Aidha, taarifa hiyo ilitaja shughuli zilizopangwa kutekelezwa na kamati ni uchambuzi wa miswada mitano ya sheria ambayo itajadiliwa na kamati nne zilizopelekewa miswada hiyo kwa mujibu wa Kanuni ya 84 (1

“Kamati ya utawala na serikali za mitaa itachambua na kujadili muswada wa sheria ya ‘Kulitangaza Jiji la Dodoma kuwa Makao Makuu ya nchi wa mwaka 2018,’’ ilisema

Pia ilisema kamati ya Katiba na Sheria itachambua na kujadili miswada miwili ambayo ni ‘Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali (na.2) wa mwaka 2018
Taarifa hiyo iliutaja muswada wa pili kuwa ni wa sheria ya Marekebisho ya sheria mbalimbali (na.3) wa mwaka 2018

“Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii itachambua na kujadili ‘Muswada wa Sheria ya Bodi ya Kitaalam ya Walimu Tanzania wa mwaka 2018’,” ilieleza

Kadhalika, Kamati ya Bajeti itachambua na kujadili ‘Musada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Ubia Kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi wa mwaka 2018,” ilisema

Pia taarifa hiyo ilisema Kamati tisa za sekta, Kamati ya bajeti na Kamati ya Masuala ya Ukimwi, zitachambua taarifa za taasisi na wizara kuhusu utekelezaji wa shughuli mbalimbali.

Taarifa hiyo ilisema kuwa kamati ya Bunge ya sheria ndogo itachambua sheria ndogo 121 zilizowasilishwa bungeni Aprili 9, mwaka huu, wakati wa mkutano wa 11 wa Bunge

“Madhumuni ni kutekeleza majukumu yake yaliyoainishwa katika kifungu cha 11 cha nyongeza ya nane ya kanuni za Bunge,” ilisema taarifa hiyo

Pia kamati ya uwekezaji wa miradi ya umma (PIC) itachambua taarifa ya uwekezaji wa taasisi, mashirika 13 kwa mujibu wa kifungu cha 12 cha nyongeza ya nane ya Kanuni za Bunge

Wabunge kujadili ripoti ya CAG Wabunge kujadili ripoti ya CAG Reviewed by KUSAGANEWS on August 19, 2018 Rating: 5

No comments: