WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamis Kigwangalla, ambaye
amelazwa katika Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI), anatarajiwa kuruhusiwa
wakati wowote baada ya afya yake kuimarika.
Hayo yalibainika jana baada ya Rais mstaafu wa awamu ya nne,
Dk. Jakaya Kikwete, kumtembelea kwa mara ya tatu kwenda kumjulia hali waziri
huyo ambaye alipata ajali ya gari akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Manyara.
Kikwete alimtembelea Kigwangalla mara ya kwanza Agosti 8,
mwaka huu alipokuwa amelazwa katika wodi ya Mwaisela na baadaye Jumatano wiki
hii akiwa kwenye wodi maalum MOI.
Jana, Rais mstaafu Kikwete alimjulia hali Kigwangalla na
kubadilishana naye mawazo akimtakia afya njema na apate nafuu ili kuendelea na
majukumu yake ya kila siku. Kikwete pia alimpongeza kwa kazi kubwa anayoifanya
katika maendeleo ya sekta ya utalii
"Nikutakie kheri. Nashukuru kwa kukukuta unaendelea
vizuri sasa na nilikuja ukiwa upo unaongea ukiwa umelala kitandani na kwa sasa
nimekuja tena umeimarika na hata kutembea na kukaa kama hivi, hongera
sana," alisema Kikwete wodini hapo.</
Jopo la madaktari bingwa wa MOI wamebainisha kuwa Dk. Kigwangalla
kwa sasa anaendelea vizuri na muda wowote anaweza kuruhusiwa kurejea nyumbani
na kwamba kwa sasa sehemu zilizobakia ni mkono wa kushoto ambao pia unaendelea
kuimarika
Hata hivyo, Dk. Kigwangalla amemweleza Kikwete kuwa kwa sasa
hali yake inaendelea vizuri na muda wowote anaweza kuruhusiwa kurejea nyumbani
huku akiendelea na mazoezi
Aidha, juzi jioni, Dk. Kigwangalla alifanya mazoezi ya
kutembea umbali wa zaidi ya kilometa moja kuanzia kwenye viunga vya hospitali
hiyo na kuzunguka maeneo yanayozunguka Muhimbili na baadae kurejea wodini kwa
kupanda ngazi kwa miguu katika jengo anamopatiwa matibabu mpaka gorofa ya sita
Waziri Kigwangalla alipata ajali ya gari Agosti 4, mwaka huu
mkoani Manyara akiwa katika ziara ya kikazi akiwa na watu sita, akiwamo Ofisa
Habari wa Wizara hiyo, Hamza Temba, ambaye alifariki dunia.
Afya ya Kigwangala yaimarika,Kutoka Moi Wakati Wowote
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 19, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment