Wakati kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge na udiwani
zikianza kesho, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema itaongeza nguvu ya
utoaji elimu kwa vyama vya siasa ili kupunguza malalamiko
NEC imetangaza kuwa Septemba 16 utafanyika uchaguzi katika
majimbo ya Monduli mkoani Arusha, Ukonga (Dar es Salaam) na Korogwe Vijijini
(Tanga) na uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata 21 zilizoko katika mikoa 10
ya Tanzania Bara
Uchaguzi katika majimbo hayo matatu unafanyika baada ya
Mwita Waitara aliyekuwa mbunge wa Ukonga na Julius Kalanga wa Monduli, wote
kuhama vyama kutoka Chadema kwenda CCM
Waitara na Kalanga wamepitishwa na CCM kuwania ubunge kwenye
majimbo yao
Jimboni Korogwe Vijijini uchaguzi unafanyika baada ya kifo
cha aliyekuwa mbunge, Stephen Ngonyani maarufu Profesa Majimarefu kilichotokea
Julai 2. CCM imempitisha Timotheo Mzava kuwania ubunge
Wagombea wa Chadema waliopitishwa kuwania ubunge ni, Asia
Msangi (Ukonga), Amina Saguti (Korogwe Vijijini) na Yonas Laiser (Monduli).
Hadi jana, ACT-Wazalendo ilikuwa ikiendelea na mchakato wa
kuwapata wagombea
Uchaguzi katika kata 21 unafanyika baada ya madiwani wengi
kujizulu kutoka vyama vya upinzani na kujiunga na CCM, wengi wakisema
wanakwenda kuunga mkono juhudi za maendeleo za Rais John Magufuli
Katika uchaguzi uliopita wa Agosti 12 uliohusisha Jimbo la
Buyungu na udiwani kwenye kata 77, yalijitokeza malalamiko yakiwamo ya mawakala
kuzuiwa kuingia kwenye vituo na fomu za wagombea kutojazwa ipasavyo
Kwa sababu hizo, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Dk Athumani
Kihamia alisema juzi kuwa wamejipanga kupunguza malalamiko na kwamba nguvu
kubwa itaelekezwa katika utoaji elimu
“Tutaongeza nguvu eneo la elimu hususan kwa vyama vya siasa
ili kupunguza malalamiko yanayojitokeza kwa kuwa huwezi kuyamaliza,” alisema Dk
Kihamia
Alisema wamebaini baadhi ya malalamiko yanatokana na elimu
ikiwamo suala la mawakala, ujazaji wa fomu za wagombea akitolea mfano wa dereva
ambaye anaweza kusababisha ajali kwa magari mengine ambayo hayakuwa na kosa
“Ni ngumu kuondoa malalamiko yote, ni kama mchezo wa mpira
wa miguu, mtu anapofungwa atatoa malalamiko iwe kwa mwamuzi au kwa nani, kwa
hiyo tunajitahidi kuongeza elimu ili kupunguza malalamiko,” alisema Dk Kihamia
NEC Kutumia Nguvu Nyingi Kutoa Elimu Kuhusu Uchaguzi
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 20, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment