Watoto wawili wameuawa
na wawazi wao kujeruhiwa kwa kupigwa kwa
nondo na kuchomwa kwa kisu sehemu
mbalimbali za miili yao kwa kile kilichoelezwa kuwa ni ugomvi wa mahari.
Tukio hilo limetokea jumamosi tarehe 18.8.2018 katika
kitongoji cha Machinjioni kijiji cha
Nyang’aranga kata ya mugeta wilayani Bunda ambapo Mwenyekiti wa kitongoji hicho
bwana Mtatiri Irondo , amesema chanzo
cha mauaji hayo ni ugonvi wa mahari kati ya
familia ya bwana magoiga mgendi na kitonyi machango.
Ametaja watoto waliouawa kuwa ni Bhoke Magoiga wa miaka
sita ,peter Magoiga mwaka mmoja na nusu,huku waliojeruhiwa ni Mary magoiga 36
pamoja na magoiga mgendi mwenye miaka 52 , tukio hilo la kikatili limefanywa
na Kitonyi Machango miaka 52.
Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji hicho bwana Paul
Marwa, amesema kuwa tokio hilo siyo mara ya kwanza kwani tukio kama hilo
liliwahi kutokea japo mtuhumiwa hakukamatwa baada ya kutoroka na kutokomea
kusikojulikana.
Diwani wa kata ya Mugeta
Mganga Jongora amesema wamelaani kitendo hicho cha kinyama na kuwasihi wananchi wasijichukulie sheria
mikononi kwa kuwa kufanya hivyo ni kukiuka sheria za nchi na haki za binadamu hasa haki ya
kuishi.
Aidha kuhusu kutoa elimu ya ukatili na unyanyasaji wa
kijinsia diwani huyo amedai kuwa wamekuwa wakitoa mara kwa mara lakini baadhi
ya watu bado hawabadiliki kwa kuacha tabia za namna hiyo, hivyo ameisihi
serikali kuwachukulia hatua kali za kisheria ili kuwa mfano kwa watu wengine.
Hata hivyo jeshi la polisi kupitia kwa Mrakibu wa polisi
ambae pia ni Mkuu wa polisi wilaya ya Bunda Imilian Kamhanda amethibitisha
kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa muuaji alitenda tukio hilo na kuuwa
mtoto mmoja papo hapo huku wa pili
akifariki njiani akipelekwa hospitalini
kupatiwa matibabu
Aidha ameongeza kwamba baada ya mtuhumiwa kutenda tukio
hilo alijichoma kisu tumboni hadi utumbo ukatoka nje lakini alisaidiwa na
wananchi waliofika katika eneo hilo na kumfunga kitamba sehemu ya jeraha na kwa
sasa anapata matibau katika hospitali teule ya bunda DDH akiwa chini ya ulinzi
wa jeshi la polisi.
Mrakibu wa polisi Kamhanda amewaomba idara ya ustawi wa
jamii kuendelea kutoa elimu katika vijiji mbalimbali ili kupunguza vitendo vya
kikatili vinavyoendelea kujitokeza wilayani hapa.
WATOTO WAWILI WAUAWA, WAZAZI WAO KUJERUHIWA KISHA MUUAJI KUJICHOMA KISU .
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 20, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment