Mawaziri mbalimbali wamefika katika Hospitali ya Taifa
Muhimbili (MNH) kumjulia hali Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi
Kigwangalla aliyepata ajali leo asubuhi Jumamosi Agosti 4, 2018
Dk Kigwangalla amepata ajali eneo la Magugu mkoani Manyara
na kupata majeraha sehemu mbalimbali mwilini
Awali, waziri huyo alipatiwa matibabu katika kituo cha
afya cha Magugu na kuhamishiwa hospitali ya Arusha Lutheran Medical Center kwa
helkopta na kisha Muhimbili
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega alikuwa wa
kwanza kufika hospitalini hapo na kufuatiwa na naibu Waziri wa Fedha na
Mipango, Dk Ashatu Kijaji na naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Dk Suzan
Kolimba
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamadi Masauni aliwasili na
viongozi mbalimbali wizara hiyo na ya Maliasili na Utalii.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dk Mpoki Ulisubisya na
mkurugenzi mtendaji wa Muhimbili, Profesa Lawrence Museru pamoja na jopo
la madaktari walimpokea Dk Kigwangalla katika kitengo cha magonjwa ya dharura
Muhimbili
Ndugu, jamaa na marafiki pia walifika hospitalini hapo
kumjulia hali waziri huyo ambaye pia ni mbunge wa Nzega Vijijini
Viongozi wamiminika Muhimbili kumjulia hali Kigwangalla
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 04, 2018
Rating:

No comments:
Post a Comment