Naibu waziri wa Elimu Sayansi na Tekolojia Mh William
Olenasha amesema serikali ya awamu ya Tano inajitahidi kuboresha Elimu kwa nchi
nzima ili kuboresha elimu kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum.
Mh Olenasha amesema hayo alipotembelea mradi wa ujenzi
wa Shule ya Sekondari ya Kisasa iliyoko Chuo cha Patandi mkoani Arusha ambapo wanafunzi
600 watasoma katika Shule hiyo wengi wao wakiwa wanafunzi wenye mahitaji maalum.
Hata hivyo amesema Kila wakati wanapojenga Shule na
miundombinu ya elimu iwe Vyuoni au Shule za Msingi lazima majengo yawe rafiki
kwa wanafunzi wenye uhitaji maalum ili iwe rahisi kwa wao kuwa kama watu
wengine.
“Hatutaki watengwe kwahiyo kama hatuwatengi kwenye jamii
hatutaki vilevile watengwe wakiwa shuleni kwa hiyo Shule hii pamoja na kuwa kwa
kiasi kikubwa itakuwa kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum lakini
watakuwepo wa kawaida kwasababu tunataka wachangayike”Alisema Olenasha
Kwa upande wa Mkuu wa Chuo hicho cha Elimu maalum
Patandi Jenasi Lenai amesema kuwa kukamilika kwa shule itasaidia wanafunzi
wenye mahitaji maalum kusoma kama wanafunzi wengine wasio na mahitaji.
Amesema kuwa kujengwa kwa majengo hayo ni kwa ajili ya
kuwachanganya pamoja wanafunzi wenye uhitaji na wasio na uhitaji ili kuwafanya
wasijisikie kama wametengwa na jamii.
Naye Mhandisi mshauri wa mradi huo Bwana Israel Mahege
amesema kuwa mradi huo wa sekondari tayari umekamili kwa asilimia 60 na
wanasubiria pesa nyingine kwa ajili ya kumalizia.
Serikali yaanza kuboresha Miundombinu ya Elimu kwa Wanafunzi wenye Uhitaji Maalum
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 01, 2018
Rating:

No comments:
Post a Comment