Mbunge CUF adai kushawishiwa kuhamia CCM


Mbunge wa Malindi (CUF), Ally Saleh  amedai Chama cha Mapinduzi (CCM) kimehamishia nguvu visiwani Zanzibar kuwashawishi wanachama wa vyama vya upinzani wajiunge nacho

Akizungumza Saleh amesema yeye ni miongoni mwa wanaoshawishiwa kujiunga na chama hicho tawala

Kabla ya kuzungumza Saleh alitoa tuhuma hizo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter huku CCM visiwani humo kikimjibu, kumtaka kutoweweseka badala yake, atulie kushuhudia wimbi la wana CUF watakaokihama chama hicho

Katika ukurasa wake huo, mbunge huyo aliandika alichoelezwa na aliyemtambulisha kuwa ni mgeni (kutoka CCM) aliyekwenda nyumbani kwake  na jinsi alivyomjibu

Saleh: Kisa kuja kwangu?

Mgeni  Sijatumwa, mimi mwenyewe

Saleh Kitu gani?

Mgeni: Tunataka uje kujiunga CCM
Saleh: Shuka ngazi haraka na mlango wa nyumba yangu usiujue

Akifafanua zaidi alipozungumza Saleh amesema, “ni kweli alikuja nyumbani kwangu, alipofika sikuwa nikimjua lakini alipoanza kujitambulisha ndio nikamjua.”

“Mtu huyo ni wa hapa Zanzibar lakini kwa sasa sitamtaja majina yake ila akibisha nitamtaja. Labda niseme tu kwamba, mimi sinunuliki, nimezaliwa upinzani na sitarajii kwenda CCM.”
Amesema alimtaka kigogo huyo kutokurudia kumshawishi kwa maelezo kuwa yeye si kama wengine wanaoshawishika

Akizungumza msemaji wa CCM- Zanzibar, Catherine Nao amemtaka Saleh kumtaja mtu huyo aliyekwenda kumshawishi, “wanaokuja CCM wanakuja si kwa ushawishi, wanakuja wao wenyewe kwa kuona mambo mazuri anayoyafanya.”

“Hakuna anayeshawishiwa, Rais Magufuli (John) yale anayoyafanya ndio anawafanya wajiunge na CCM, lakini niseme tu, Septemba 15, 2018 tukiwa tunazindua kampeni za uwakilishi wa Jang’ombe, kuna wana CUF wengi watajiunga na CCM, subirini mtaona.”
Mbunge CUF adai kushawishiwa kuhamia CCM Mbunge CUF adai kushawishiwa kuhamia CCM Reviewed by KUSAGANEWS on August 01, 2018 Rating: 5

No comments: