Rais John Magufuli ataja sababu za kumteua Kafulila


Rais John Magufuli ameeleza sababu za kumteua David Kafulila kuwa katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe kuwa ni jinsi alivyopambana katika kashfa ya akaunti ya Tegeta Escrow iliyohusu kampuni ya Independent Power Tanzania Ltd (IPTL).

Rais ameyasema hayo leo Agosti Mosi wakati akiwaapisha makatibu wakuu, manaibu katibu wakuu, makatibu tawala na wakuu wa mikoa

“Ndugu yetu Kafulila alipokuwa huko kwenye chama chake alipigania suala la IPTL, nani anayeipenda IPTL tulivyofanyiziwa? Uwe CCM uwe Chadema uwe CUF uwe huna chama, suala la IPTL halina chama,”

 “Lakini alisimama akapingwa, akaitwa tumbili akaitwa nani wala hajageuka kuwa tumbili ni huyu huyu. Huyu siyo mpianzani bali ni mtekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi,” amesema Rais Magufuli

Amewataja baadhi ya viongozi wakiwamo makatibu tawala na kusema lakini aliyekuwa mpinzani ni Kafulila peke yake, huku kwa wakuu wa wilaya akisema wapo watatu na nusu

“Ukingalia ma-RAS, aliye cross chama ni mmoja tu, Kafulila, katika 13 wote. Ukienda kwa Ma-DC wako 31, niliowakuta nafikiri ni watatu na nusu walio cross vyama vingine. Kuna huyo wa Dodoma (Katambi) mjini, Longido, kuna wa Nanyumbu nafikiri Machali na Bukombe ambaye ndiyo naita nusu (Nkumba) ambaye alikaa CCM kule akahamia upinzani siku tatu akarudi huku,” amesema

Rais amesema lengo lake ni kujenga nchi yenye umoja, isiyo na ubaguzi wa dini, kabila wala vyama na yuko tayari kuwashirikisha wote wanaotaka kupeleka mbele nchi
Rais John Magufuli ataja sababu za kumteua Kafulila Rais John Magufuli ataja sababu za kumteua Kafulila Reviewed by KUSAGANEWS on August 01, 2018 Rating: 5

No comments: