Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albart Chalamila amesema ni fedheha na
aibu kwa madiwani kuingia kwenye vikao vya kujadili maendeleo ya halmashauri
zao huku wakiwa na mihemko ya itikadi za siasa za vyama vyao
Amesema vyama vya siasa si ugomvi, kwamba Chama cha
Mapinduzi (CCM) na viongozi wake wana wajibu wa kupokea ushauri wote mzuri
kutoka upinzani na kuufanyia kazi kwa ajili ya maendeleo ya Mkoa huo na sio
kubeza
Ametoa kauli hiyo leo Jumamosi Agosti 18, 2018 mjini
Rujewa kwenye kikao maalumu cha baraza la madiwani la halmashauri ya Wilaya ya
Mbarali kilichoketi kwa ajili ya kujibu hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa
Hesabu za Serikali (CAG).
Amewataka madiwani wa Mkoa wa Mbeya kuacha tabia ya kusongwa
na mihemko ya kisiasa ambayo hazisaidii maendeleo ya halmashauri na kata
wananaziongoza
Amesema kuendekeza siasa za aina hiyo kunadhoofisha ukuaji
wa uchumi wa Mkoa huo na wananchi wake
Amebainisha kuwa anakaribisha maoni na atayapokea bila
ubaguzi, kusisitiza kwamba atakayepekea maoni hayo ahakikishe yawe ya kujenga
na si majungu
“Kwa lugha nyepesi mnapongia hapa ndani kwa ajili ya
kujadili mustakabali wa halmashauri hii (Mbarali) ni kitendo cha fedheha kama
mtaingia mkiwa na mihemko ya itikadi ya vyama vya kisiasa,” amesema
“Narudia tena ili tuijenge Mbarali na Mbeya yetu,
madiwani wa Chadema na wa CCM mnaitwa madiwani wa Serikali ya Tanzania
na wajibu wenu ni mmoja tu kuwawakilisha wananchi kwa hoja imara na
kuisimamia Serikali yenu iweze kufanya vitu vyake vizuri.”
RC Mbeya afunguka, ataka mawazo mazuri ya wapinzani kupokelewa
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 18, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment