Maofisa watatu wa halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo mkoani
Kagera wamesimamishwa kazi na mkuu wa Mkoa huo Brigadia Jenerali Marco Gaguti
Amechukua uamuzi huo ili maofisa hao wapishe uchunguzi wa
upotevu wa zaidi ya Sh600 milioni ambazo hazikuwakilishwa kama mapato ya
halimashauri kuanzia 2016 hadi 2018
Hayo yamebainika jana Ijumaa Agosti 17, 2018 katika kikao
maalum cha Kamati ya fedha na mipango ya halmashauri hiyo cha kujadili
taarifa ya kamati iliyoundwa na aliyekuwa mkuu wa Mkoa huo
Waliosimamishwa kazi ni Alexander Bashaula ambaye ni mweka
hazina wa halmashauri hiyo, Salanga Mahendeka (mhasibu) na Emanuel Maleo
ambaye ni ofisa ushirika, wote wakituhumiwa kupoteza fedha na
kukiuka viapo vya uaminifu
Katika kikao hicho mkuu huyo wa Mkoa amesema zaidi ya Sh690
milioni hazikuwasilishwa kama mapato ya halmashauri kuanzia Agosti 2016
hadi Mei 2018, Sh 427 milioni hazikuwasilishwa benki na wakusanya mapato
“Baada ya uchunguzi wa kamati ya katibu tawala
wa mkoa wa Kagera hivi karibuni ilibainika kuwa mwenendo wa ukusanyaji wa
mapato haulidhishi na tunachukua hatua kwa wanaopoteza fedha za umma”
alisema
Ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa
(Takukuru) kuanza kuchunguza ubadhilifu huo wa mali ya umma pamoja
na kufuatilia wote kwa ajili ya kuchukuliwa hatua za kisheria
Maafisa 3 wapewa Off Kwa Ubadhirifu wa Fedha za Magufuli Zaidi ya Sh Milioni 600
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 18, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment