RC Aagiza Wananchi Kuwekwa Ndani


Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila, ameliagiza Jeshi la Polisi kuwakamata na kuwasweka ndani wananchi wote wa Kijiji cha Ngole katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya kwa kosa la kuvamia na kuvunja mradi wa maji wa kijiji cha jirani cha Mashesye

Chalamila anetoa agizo hilo leo wakati wa Kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya cha kupokea Taarifa ya Mthibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) baada ya Mwenyekiti wa Kijiji cha Mashesye na Diwani wa Kata ya Ilungu kuwasilisha taarifa ya uhalifu uliofanywa na wananchi hao

Viongozi hao walimweleza Chalamila kuwa wananchi hao walivunja banio na kukatakata mabomba yaliyokuwa yametandazwa na kwamba mradi huo umegharimu zaidi ya shilingi milioni 27

RC Aagiza Wananchi Kuwekwa Ndani RC Aagiza Wananchi  Kuwekwa Ndani Reviewed by KUSAGANEWS on August 15, 2018 Rating: 5

No comments: