Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila, ameliagiza
Jeshi la Polisi kuwakamata na kuwasweka ndani wananchi wote wa Kijiji cha Ngole
katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya kwa kosa la kuvamia na kuvunja mradi wa
maji wa kijiji cha jirani cha Mashesye
Chalamila anetoa agizo hilo leo wakati wa Kikao cha Baraza
la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya cha kupokea Taarifa ya Mthibiti
na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) baada ya Mwenyekiti wa Kijiji cha
Mashesye na Diwani wa Kata ya Ilungu kuwasilisha taarifa ya uhalifu uliofanywa
na wananchi hao
Viongozi hao walimweleza Chalamila kuwa wananchi hao
walivunja banio na kukatakata mabomba yaliyokuwa yametandazwa na kwamba mradi
huo umegharimu zaidi ya shilingi milioni 27
RC Aagiza Wananchi Kuwekwa Ndani
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 15, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment