Rais John Magufuli amewasili jijini Mwanza leo Jumamosi
Agosti 18, 2018 kwa ndege ya Dreamliner akitokea jijini Dar es Salaam
Katika safari hiyo kiongozi mkuu huyo wa nchi alizungumza na
abiria waliopanda ndege hiyo na kupiga nao picha mbalimbali
Baada ya kuwasili, Rais Magufuli alikwenda katika Hospitali
ya Rufaa ya Bugando akapopokewa na viongozi kadhaa akiwemo Mkuu wa Mkoa wa
Mwanza, John Mongella
Wakati akitoka katika hospitali hiyo alisimamisha msafara
wake na kuzungumza na wanafunzi wa Shule Msingi Mongella iliyopo eneo la
Bugando waliokuwa wamesimama pembeni mwa barabara
"Mmekuja kufanya nini hapa," Rais Magufuli
aliwauliza swali wanafunzi hao
Kwa sauti ya pamoja, wanafunzi hao wakajibu "Tumekuja
kukuona"
Baada ya jibu hilo, Rais Magufuli aliwashukuru wanafunzi hao
na kuwaambia, "Nitarudi siku nyingine kuonana na kuzungumza nanyi. Leo
nimefika hapa kumuona mgonjwa wangu ambaye amelazwa hapa hospitalini. Endeleeni
kuwaombea wagonjwa waliolazwa hospitalini.”
Baada ya kumaliza kuzungumza na watoto hao aliondoka eneo
hilo
Rais Magufuli awasili Mwanza na Dreamliner, atembelea Bugando
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 18, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment