Kwa mara ya kwanza Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi wa CUF
Profesa Ibrahim Lipumba amezungumza na wafuasi wa CUF kisiwani Unguja tangu
chama hicho kuwa na mgogoro.
Mgogoro huo ambao umedumu kwa muda wa miaka miwili
sasa na kupelekea wafuasi wa chama hicho kugawika pande mbili ambapo upande
mmoja unamunga mkono katibu Mkuu Maalim Seif Sharif Hamad na wengine
wanaomuunga mkono Mwenyekiti Profesa Lipumba.
Akizungumza katika mkutano ambao haukuungwa mkono na wafuasi
wa chama hicho wanaomuunga mkono Maalim Seif, Profesa Lipumba amesema kuwa
hakuna wa kiongozi wa CUF alieshiriki kutetea haki ya wazanzibar kuliko
yeye
Amesema mwaka 2001 alipigwa na kuumizwa kwa kudai haki ya
wazanzibari kwa kupinga matokeo ya uchaguzi wa Zanzibar mwaka 2000
"Nilipigwa na kuvunjwa mkono wangu kutokana na
kuwahamasisha wananchi maandamano ya amani ya kudai matokeo halali ya uchaguzi
wa 2000 na kudai katiba ya Tanzania "amesema.
Alieleza kuwa katika wanasiasa wa Tanzania yeye ndie
kiongozi pekee aliyemstari wa mbele kupigania haki na maslahi ya
wazanzibari ndani ya serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
Prof Lipumba atinga Zanzibar kwa Maalim Seif
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 16, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment