Mhasibu Chuo cha Ustawi wa jamii atupwa jela miaka mitano


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuhukumu kifungo cha miaka mitano jela aliyekuwa Mhasibu wa Chuo cha Ustawi wa Jamii, Gryson Mnyawami baada ya kupatikana na hatia ya wizi wa zaidi ya Sh9 milioni akiwa mtumishi wa umma

Hakimu Mkazi Mkuu, Janeth Mtega ametoa hukumu hiyo leo Agosti 16 baada ya kupitia ushahidi wa mashahidi watano wa upande wa mashtaka ambao walithibitisha wizi huo pasipo kuacha shaka.

 Wakili wa Serikali Janeth Magoho ameieleza mahakama kuwa mshtakiwa huyo ni mkosaji wa kwanza na hakuna kumbukumbu za makosa mengine

Hata hivyo, Magoho aliiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa mshtakiwa huyo kwa kuwa kitendo cha wizi alichofanya  akiwa  mtumishi wa umma ni kibaya na  kinaitia hasara  Serikali

Ameongeza kuwa, suala la wizi katika Chuo cha ustawi limekuwa likitokea mara kwa mara

“Kitendo hicho ni kudhulumu wanafunzi na kwamba siyo cha haki kwani ile fedha ni fedha ya walipa kodi hivyo adhabu kali itakuwa fundisho kwake na kwa wengine wenye tabia kama hiyo,”amesema

Mnyawami katika utetezi wake aliiomba mahakama hiyo kumpunguzia adhabu na alikubali kulipa fedha hizo taratibu lakini taasisi ndiyo ilimkatalia

Ameongeza kuomba apunguziwe adhabu kwa  kuwa dada yake ni mgonjwa na mama yake ni mjane na wote wanamtegemea yeye.
Baada ya kusikiliza hoja hizo Hakimu Mtega alimuhukumu mshtakiwa huyo kifungo cha miaka mitano jela

Mhasibu Chuo cha Ustawi wa jamii atupwa jela miaka mitano Mhasibu Chuo cha Ustawi wa jamii atupwa jela miaka mitano Reviewed by KUSAGANEWS on August 16, 2018 Rating: 5

No comments: