Kampuni ya Bakhressa Yasubiri Muongozo ya TCRA


Uongozi wa Kampuni ya Bakhressa (BFPL) umesema unasubiri kwa hamu mwongozo utakaotolewa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)   kuhusu ving'amuzi vilivyoondoa chaneli za ndani baada ya kukiuka masharti ya leseni

Agosti 13 mwaka huu, Waziri wa Habari, Sanaa,Michezo,Burudani na Wasanii,Dk Mwakyembe aliitaka TCRA kutoa mwongozo  utakaosadia kampuni za visimbuzi za Azam, Zuku na DSTV zitakavyoweza kurusha maudhui ya ndani

Hivi karibuni kampuni hizo zililazimika kuacha kurusha chaneli za ndani baada ya kukiuka masharti ya leseni zao ambayo yanawataka kurusha maudhui hayo kwa kuyalipia

Meneja Uhusiano wa Bakhressa, Hussein Sufian ameiambia Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, leo Alhamisi Agosti 16, 2018 kuwa wanausubiri mwongozo huo

Kamati hiyo ya Bunge imeelezwa hayo wakati ilipotembelea kiwanda cha kusindika matunda na kutengeneza juisi kilichopo Mlandenge wilayani Mkuranga

Sufian ameeleza hayo wakati akitoa changamoto zinazoikabili kampuni hiyo na kusema hatua ya Serikali ya kuzitaka Azam kuondoa maudhui ya chaneli za ndani ni kuwaumiza wananchi

"Tunausubiri kwa hamu mwongozo huu ili wananchi wetu waondokane na hali ya kumiliki visimbuzi viwili jambo ambalo ni mzigo kwao

“Tunaamini busara itatumika zaidi kurejesha huduma kwa Watanzania na muafaka utapatikana wa suala hili na tuna imani na Serikali," amesema Sufiani
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara na Uwekezaji, Mhandisi Stella Manyanya amesema wizara hiyo imelisikia jambo hilo na wanalifuatilia kwa ukaribu kwa sababu linahusu biashara

"Tutalifuatilia ili kujiridhisha na hatimaye tupate muafaka. Sasa hivi popote panapohusu biashara lazima tufuatilie na hili la visimbuzi ni biashara pia," amesema Manyanya

Kampuni ya Bakhressa Yasubiri Muongozo ya TCRA Kampuni ya Bakhressa Yasubiri Muongozo ya TCRA Reviewed by KUSAGANEWS on August 16, 2018 Rating: 5

No comments: