Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetoa ufafanuzi juu ya
madai ya Ubalozi wa Marekani kuhusu uchaguzi mdogo wa Agosti 12
Katika taarifa iliyotolewa leo Agosti 15, 2018 NEC imeutaka
ubalozi huo uthibitishe inachokieleza juu ya uchaguzi mdogo wa Jimbo la
Buyungu na kata 36 ikisema uchaguzi mdogo huwa hauna waangalizi wa kimataifa na
kuhoji ubalozi huo umetoa wapi taarifa hizo na hayo ulioyaona ni kwa kutumia
utaratibu upi na sheria ipi
“Katika Jimbo la Buyungu mgombea wa ubunge mmojawapo
(Chadema) alijitokeza kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii
akaeleza hisia zake na kusema bayana kuwa amekubaliana na matokeo na ameshukuru
kwa kuwa uchaguzi huo umemjenga,” inasema taarifa hiyo na kuongeza
“Kilichotokea Arusha
ni vurugu mitaani mbali na maeneo ya vituo vya kupigia kura, kwa kuwa vurugu
hizo zilipelekea jinai kufanyika vyombo husika vinashughulikia. Hakuna chama
chochote kilichojitokeza kusema na kuthibitisha kuwa uchaguzi haukuwa huru na
haki,” inasema taarifa hiyo iliyosainiwa na ofisa habari mwandamizi wa NEC,
Christina Njovu
“Tume ya Taifa ya Uchaguzi inapenda kuufahamisha umma kuwa
Tanzania ni nchi huru na inaendesha chaguzi zake kwa mujibu wa Katiba yake na
sheria za uchaguzi.”
NEC yajibu taarifa ya ubalozi wa Marekani kuhusu Uchaguzi Mdogo
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 15, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment