Dar es Salaam. Siku chache baada ya wabunge wawili wa
Chadema kutangaza kujiuzulu nyadhifa zao na kuhamia CCM, madiwani wengine
wawili wa chama hicho wametangaza kufuata nyayo zao
Wiki iliyopita mbunge wa Ukonga (Chadema), Mwita Waitara
alitangaza kujiunga na CCM na Julai 31 usiku, mbunge wa Monduli kupitia chama
hicho, Peter Kalanga alitangaza kujiuzulu wadhifa huo na kutimkia CCM
Juzi, Diwani wa Vingunguti (CUF), Omary Kumbilamoto
alijiuzulu huku akitaja sababu nne zilizomfanya kuchukua uamuzi huo ikiwamo
mgogoro ndani ya chama chake. Kumbilamoto pia alikuwa naibu meya wa Manispaa ya
Ilala
Hata hivyo, jana diwani wa Kizota jijini Dodoma (Chadema),
Jamala Ngalya alijiuzulu na kuhamia CCM
Sababu nne za Kumbilamoto
Kumbilamboto alitangaza uamuzi wa kujiuzulu na kutaja sababu
nne ikiwamo mgogoro ndani ya CUF unaomkwaza kutekeleza majukumu yake.
Pia alisema viongozi
wa CUF walishindwa kujitokeza katika kata yake kumsaidia lilipotokea janga la
mafuriko mwaka huu
Sababu nyingine ameitaja kuwa ni kupewa vitisho vya
kufukuzwa uanachama kwa kile alichodai kuwa karibu na mkuu wa Mkoa wa Dar es
Salaam, Paul Makonda
Akifafanua sababu hizo, Kumbilamoto ambaye anamuunga mkono
katibu mkuu wa CUF, Maalim Seif ameufananisha mgogoro ndani ya chama hicho na
ule wa mataifa ya Palestina na Israel ambao umekosa suluhu
“Mvutano huo umesababisha nishindwe kutimiza wajibu wangu
kwa ufanisi huku napewa vitisho vya kufukuzwa uanachama kwa sababu ya kuwa
karibu na viongozi wa Serikali akiwamo mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul
Makonda,” alisema
Alisema wakati Kata ya Vingunguti ilipokumbwa na mafuriko
hakuna kiongozi wa CUF aliyekwenda kutoa msaada wala kuitembelea isipokuwa
uongozi wa Serikali wa mkoa
“Sikuletewa hata kijiko na viongozi wangu wa chama, lakini
viongozi wa Serikali walinisaidia. Hata hivyo upande wangu wa chama unaniambia
mimi ni msaliti kutokana na ushirikiano ninaoupata (serikalini),” alisema
Alisema wakati wowote atafanya mkutano wa hadhara kuwaeleza
wananchi wa kata hiyo chama anachokwenda kufanyia shughuli zake za kisiasa na
amewaachia wana CUF chama chao
Meya wa Ilala, Charles Kuyeko alisema, “nimesikia kama
ulivyosikia wewe, lakini hajaniaga na wiki nzima nilikuwa namtafuta simpati.”
Wakati huohuo, diwani wa Kizota (Chadema), Ngalya ametangaza
kujiuzulu wadhifa huo na kujiunga na CCM
Akizungumzia uamuzi huo, Ngalya alisema anarudi nyumbani kwa
kuwa waliomkata wakati wa Uchaguzi Mkuu 2015 ndani ya CCM kwa sasa hawapo
madarakani
Diwani huyo ambaye hivi karibuni alichaguliwa kuwa mnadhimu
wa madiwani wa Chadema Tanzania, alisema uamuzi wake ni ‘huru’ na anaungana na
timu ya Rais John Magufuli ili kuchapa kazi.
Naibu meya Ilala ataja sababu za kuhama CUF, madiwani waendelea kutimka
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 02, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 02, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment