Waziri Kairuki aahidi mazingira mazuri kwa wachimbaji wadogo


Waziri wa Madini Angellah Kairuki amesema serikali itaendelea kuweka mazingira mazuri kwa wachimbaji wadogo nchini kunufaika ili iweze kukusanya kodi zitakazotumika kwenye shughuli za maendeleo

Ametoa kauli hiyo leo Agosti 2 wakati akizungumza na wachimbaji wadogo wa madini aina ya Green Garnet eneo la Lemshuku katika Kijiji cha Komoro wilayani Simanjiro mkoa wa Manyara

Amesema lengo la kuwajengea uwezo wachimbaji wadogo ni kuwapa nguvu ya kukua kutoka wachimbaji wadogo hadi wachimbaji wa kiwango cha kati hatua itakayoongeza mapato na ajira.

Kairuki amesema serikali inakamilisha  mchakato wa  kurejesha ruzuku kwa wachimbaji wadogo uliokua umesitishwa baada ya kubainika sio wote waliokua wakinufaika walikua wachimbaji wadogo

"Serikali inaamini kupitia ruzuku tutakayoanza kuitoa kwa wachimbaji wadogo ambao hawana uwezo wa kifedha watanufaika ipasavyo, lengo sio mbaki wachimbaji wadogo siku zote,” amesema Kairuki.

Amesema mchango wa sekta ya madini nchini ni asilimia 4.7 kiwango ambacho ni kidogo ukilinganisha na wingi rasilimali hiyo na nguvu kazi ya vijana wanaoweza kuwa kwenye sekta ya madini

Ameongeza kuwa serikali imeshabainisha maeneo 44 kwaajili ya wachimbaji wadogo nchini na utaratibu wa kuyatoa utafanyika kwa kufuata taratibu
Mwenyekiti wa chama cha ushirika  wa wachimbaji  wadogo Lemshuku(Komisco),Salehe Abdallah amesema ushirika wao una jumla ya wachimbaji wadogo 250 na wamekua wakitoa michango mbalimbali ya elimu katika shule ya Msingi ikiwamo ujenzi wa madarasa mawili na nyumba moja ya walimu

Waziri Kairuki aahidi mazingira mazuri kwa wachimbaji wadogo Waziri Kairuki aahidi mazingira mazuri kwa wachimbaji wadogo Reviewed by KUSAGANEWS on August 02, 2018 Rating: 5

No comments: